Ujumbe wa Hizb ut Tahrir Uko Wazi Kabisa na Si Tishio kwa Usalama
- Imepeperushwa katika Kenya
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Chama cha Kisiasa cha Kiislamu cha Hizb ut Tahrir Kenya kimesikitishwa sana na hatua iliyochukuliwa na vyombo vya usalama nchini Kenya kusitisha Kongamano lao jijini Mombasa. Kongamano hilo chini ya kauli mbiu "Khilafah Tuitakayo kwa Njia ya Utume" lililo andaliwa kufanyika mnamo Jumapili 8 Mei 2016 kuanzia saa nane mchana hadi saa kumi jioni lilisimamishwa dakika ya mwisho kwa madai ya 'sababu za kiusalama'.