Urasilimali Umezigeuza Hospitali kuwa Mapango ya Mauti!
- Imepeperushwa katika Kenya
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mgomo unaoendelea wa madaktari na wauguzi sasa unaingia wiki yake ya pili, ukiwaacha wagonjwa wasio na hatia kufariki bila ya huduma katika hospitali zote za umma. Lengo kuu nyuma ya mgomo huu, ni kuilazimisha serikali kutekeleza makubaliano ya 2013 ya kuwalipa madaktari mabaki ya malipo yao pamoja na nyongeza ya asilimia 300 kwa mishahara yao.