Jumapili, 19 Shawwal 1445 | 2024/04/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Al-Waqiyah TV: Je, Upigaji Marufuku wa Abayah wa Ufaransa Unasema Nini Kuhusu Usekula?

[Al-Waqiyah TV]
Je, Upigaji Marufuku wa Abayah wa Ufaransa Unasema Nini Kuhusu?!

Serikali ya Ufaransa imeanzisha marufuku ya uvaaji wa Abayah katika shule za Ufaransa, ambayo ilianza kutekelezwa mwezi huu wa Septemba. Ilisema kwamba mavazi ya kidini yanahujumu kanuni za kisekula zinazounda msingi wa dola yake, na kutoegemea upande wowote wa kidini ndani ya shule. Abayah pia inajulikana kama Jilbab, na ni nguo pana na ndefu ambayo huvaliwa juu ya nguo za nyumbani wakati mwanamke wa Kiislamu anaingia kwenye maisha ya umma. Uamuzi huo unajiri baada ya miezi kadhaa ya mijadala juu ya suala hilo na wito kutoka upande mkali wa kulia kutoa marufuku.

Hivyo ni kwa nini haswa serikali ya Ufaransa imeanzisha marufuku hii wakati huu? Je, ni kipi kilicho nyuma ya Wafaransa kupagawishwa na vazi la Kiislamu? Na marufuku kama hiyo inasema nini kuhusu itikadi na mfumo wa kisekula ambao dola ya Ufaransa na dola nyengine nyingi ulimwenguni zinaegemea juu yake?

Mjadala huu unatarajia kushughulikia maswali haya na mengine yanayohusiana na mada hii.

#France #AbayahBan #Hijab #Islam #Secularism

Jumamosi, 01 Rabi-ul Awwal 1445 H sawia na 16 Septemba 2023 M

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu