Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari 28/09/2022

Vichwa vya Habari:

Erdogan to Kusawazisha Mahusiano na Syria

Bomba la Gesi la Urusi Lashambuliwa

Urusi Yazingatia Kufunga Mpaka

Maelezo:

Erdogan to Kusawazisha Mahusiano na Syria

Vyombo vya habari vya Uturuki vimeripoti kuwa Rais Recep Tayyip Erdogan aliwaambia wanachama wa chama chake kwamba alisikitishwa na kukosa nafasi ya kukutana na Rais wa Syria Bashar al-Assad katika Mkutano wa hivi karibuni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai mapema mwezi Septemba. Kauli ya Erdogan ilifuatia ripoti kwamba mkuu wa ujasusi wa Uturuki amekuwa akikutana na mwenzake wa Syria hivi majuzi katikati mwa Septemba. Msimamo wa Erdogan haujawahi kuweka juu ya Syria na umekuwa ukibadilika mara kwa mara, wakati Erdogan akizungumzia kuondolewa kwa Bashar al-Assad hatimaye aliondoka kwenye maneno kama hayo. Lakini tangu Imarati kuwa mwenyeji wa al-Assad jijini Dubai mnamo 2021, na tangu Misri itoe wito wa Syria kuingia tena katika Jumuiya ya Waarabu, matamshi ya Erdogan pia yamebadilika. Erdogan sasa anahama kutoka kukubali kisiri hadi kufungua ushirikiano na Bashar al-Assad. Huku Erdogan akijionyesha kama mwokozi wa Waislamu kote duniani, siasa zake ziko mbali sana na hilo.

Bomba la Gesi la Urusi Lashambuliwa

Wataalamu wa matetemeko ya ardhi wameripoti milipuko chini ya maji ya Bahari ya Baltic huku uvujaji ukitokea kwenye bomba la gesi la Nord Stream. Opareta wa Nord Stream 1 alisema njia za chini ya bahari zilikuwa na uharibifu "usio na kifani" kwa wakati mmoja. Huku maopareta wa Nord Stream 2 wakionya juu ya kupotea kwa presha ndani ya bomba hilo ambayo ilisababisha onyo kutoka kwa mamlaka za Denmark kwamba meli zinapaswa kuepuka eneo karibu na kisiwa cha Bornholm. Tuhma zilianza mara moja huku Ukraine ikiilaumu Urusi kwa kushambulia bomba lake lenyewe, bomba ambalo Urusi ililifunga wiki mbili zilizopita. Urusi iliilaumu Ukraine, lakini Ukraine ina mabomba ya Urusi yanayopitia eneo lake ambayo itakuwa rahisi sana kuyahujumu. Matokeo yote yale. Hili litakuwa shambulizi la kwanza kwa miundombinu nje ya ukumbi wa vita. Kichocheo kikubwa.

Urusi Yazingatia Kufunga Mpaka

Mamlaka za Urusi zinaripotiwa kuzingatia kufunga mpaka wa nchi hiyo. Tangu kutangazwa kwa sehemu ya uhamasishaji wengi wanaoingia katika kigawanyo hiki wamejaribu kuondoka nchini. humo Urusi ina hitaji kubwa la wanajeshi kwani inahitaji kushikilia mstari nchini Ukraine. Lakini tangu kupotea kwa Kharkiv, Urusi sasa inayaunganisha majimbo ya Mashariki mwa Ukraine, Urusi itahitaji wanajeshi kuyashikilia maeneo haya. Ufanisi wa wanajeshi waliohamasishwa ni wa kutilia shaka kwani watakuwa na ari ya chini na hivyo kuwa wanajeshi wasio na ufanisi.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu