Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Kombe la Dunia la Qatar linaonyesha kwamba Ummah wa Kiisilamu uko katika bonde moja, Huku watawala wake wenye Kuhalalisha Mahusiano wako Bonde Jengine
(Imetafsiriwa)

Habari:

“Mwanadiplomasia wa Kiyahudi alionyesha wasiwasi wake juu ya kukosekana uhalalishaji mahusiano na makubaliano ya amani, yaliyotiwa saini na umbile la Kiyahudi pamoja na baadhi ya watawala wa nchi za Kiarabu, na watu wa nchi hizo. Ilionekana wazi katika Kombe la Dunia nchini Qatar kwamba watu wanakataa uhalalisha mahusiano na mvamizi huyo.” (Arabic 21)

Maoni:

Hakika, Palestina imefungwa madhubuti na Iman wa Waislamu, kwani ndio mahali pa Israa ya Mtume na Qiblah chao cha kwanza. Kuhusu fadhila na hadhi yake, Hadith zilisimuliwa kutoka kwa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (saw). Ardhi yake ilinyweshezwa kwa damu ya washindi na wakombozi. Kutokana na hayo, Makhalifa na Masultani wa Waislamu waliilinda Palestina, wakikataa kujadili juu yake, au kukata tamaa, hata shubiri yake moja. Muhanga na ushujaa zimetolewa, na zingali zinatolewa, kupitia mapenzi ya Palestina na katika utetezi wake.

Hivi ndivyo ilivyo, licha ya usaliti wa watawala wa Waislamu na uhalalishaji wao wa mahusiano na umbile la Kiyahudi, watu hawakuyahalalisha nalo. Badala yake wanachukulia uhalalisha mahusiano kuwa ni usaliti na uhalifu mkubwa. Hata vijana walijiondoa kwenye mashindano hayo ya michezo, kwa sababu wapinzani wao walikuwa kutoka kwa umbile la Kiyahudi. Leo, katika kivuli cha Kombe la Dunia, na licha ya usaliti wa Qatar kwa kuwaruhusu Mayahudi kuingia Qatar kuhudhuria Kombe la Dunia, na kuanzishwa kwa ndege ya moja kwa moja kati ya umbile la Kiyahudi na Qatar kwa usafirishaji wao, na licha ya kuruhusu vyombo vyake vya habari na waandishi wao Kuwa huko kupeperusha Kombe la Dunia, watu walikataa kuzungumza nao. Video nyingi zinazoonyesha kukataa huku zimesambaa mitandaoni, kufikia kiasi ambacho baadhi ya waandishi wa habari hawa kulazimika kusema uwongo na kujificha, kwamba ni kutoka nchi nyingine, ili kukwepa ghadhabu ya watu!

Mapenzi ya Palestina, na utetezi wake, lazima yaelezwe vizuri. Mapenzi kwa Palestina haimaanishi kuwa watu wanyanyua bendera ya ukoloni, “bendera ya kitaifa ya Palestina,” viwanjani. Haimaanishi kuwa wavae kitambaa cha keffiyeh, au kwamba washangilie kwa ajili ya Palestina na kuimba nyimbo za kitaifa kwenye stendi na viwanja. Inamaanisha watu lazima walaani mahusiano yaliyowekwa na watawala pamoja na umbile hili halifu, kulipatia ulinzi. Inamaanisha kwamba watu lazima waachane na mgawanyiko na mipaka ya bandia, iliyowekwa na watawala hawa na mabwana zao wa kikoloni, ili kuzigawanya nchi za Waislamu. Hii ni ili Waislamu waungane chini ya bendera ya “Hapa Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Hii inamaanisha kuwa juhudi zilenge kusimamisha dola itakayoikomboa Palestina na kuliondoa umbile hili vamizi, na hivyo kutimiza ahadi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) ya kuwashinda Mayahudi na kuikomboa Palestina.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema,

«لَا تَقُومُ السَّاعَةُ حَتَّى يُقَاتِلَ الْمُسْلِمُونَ الْيَهُودَ، فَيَقْتُلُهُمْ الْمُسْلِمُونَ، حَتَّى يَخْتَبِئَ الْيَهُودِيُّ مِنْ وَرَاءِ الْحَجَرِ وَالشَّجَرِ، فَيَقُولُ الْحَجَرُ أَوْ الشَّجَرُ: يَا مُسْلِمُ يَا عَبْدَ اللَّهِ، هَذَا يَهُودِيٌّ خَلْفِي فَتَعَالَ فَاقْتُلْهُ، إِلَّا الْغَرْقَدَ فَإِنَّهُ مِنْ شَجَرِ الْيَهُودِ» 

“Kiyama hakitasimama hadi Waislamu watapigana na Mayahudi, na Waislamu watawaua, mpaka Myahudi atajificha nyuma ya jiwe au mti, na jiwe au mti huo utasema, ‘Ewe Muislamu, Ewe mja wa Mwenyezi Mungu, kuna Myahudi nyuma yangu; njoo umuue; Isipokuwa mti wa Gharqad hautasema, kwa kuwa ni mti wa Mayahudi.’” [Imepokewa na Muslim] Na tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) kwamba hili litakuwa karibuni, kupoza nyoyo za waumini.

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na
Baraa'a Manasrah

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu