Jumapili, 22 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Jibu la Swali: Kuamiliana na Dola zilizo za Kivita Kivitendo

Ndugu mmoja aliniuliza kuhusu kufanya kazi katika kiwanda cha kutengeneza makontena katika makaazi ya Barkan. Hivi majuzi, sehemu ya kiwanda hiki iligeuzwa kwa manufaa ya jeshi la ‘Israel’, na kinatengeneza matrela ya kusafirisha majenereta ya umeme na vitu vyengine vinavyohusiana na jeshi. Je, inajuzu kufanya kazi katika sehemu hii inayotengeneza matrela kwa ajili ya jeshi?

Kwa Maongezi Matamu, Yenye Sumu kuhusu Mustakabali wa Lebanon na Kanda! Mjumbe wa Marekani Tom Barrack yuko nchini Lebanon Kuimarisha Kukamilishwa kwa Makubaliano ya Amani na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi!

Mnamo Julai 7, 2025, katika mkutano na waandishi wa habari katika Kasri la Rais, Mjumbe wa Marekani Tom Barrack alitoa taarifa akisema kwamba "Lebanon na kanda hii wana fursa nzuri ambayo lazima ichukuliwe," kwamba "wakati umefika wa kubadilisha kanda hii," na kwamba "kila mtu amechoshwa na kile kilichotokea," kama alivyoweka. Pia alisema kwamba "usalama utavutia uwekezaji kwa Lebanon," kwamba "Rais wa Marekani alithibitisha dhamira yake ya kuchangia kujenga amani na ustawi nchini Lebanon," na kwamba "fursa inapatikana kwa Walebanoni kuifanya nchi yao kuwa Lulu ya Mashariki kwa mara nyingine tena."

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu