Jumamosi, 21 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/13
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Matukio ya Umwagaji damu huko Sweida Yafichua Hatari za Makundi Yenye Uhusiano wa Kigeni Uhalalishaji Mahusiano ni Jinai Inayohujumu Miaka 14 ya Muhanga wa Mapinduzi

Kufuatia siku kadhaa za mapigano makali yaliyogharimu maisha ya mamia ya ndugu zetu waliokufa shahidi, Wizara ya Ulinzi ghafla na kwa mshtuko ilitangaza Jumatano kuwa ni siku ya kuanza kujiondoa kwa jeshi la Syria katika mji wa Sweida. Haya yanajiri baada ya wito wa Marekani wa kuondoa vikosi vya serikali katika jimbo hilo na msururu wa mashambulizi makali ya anga yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi mjini Damascus siku ya Jumatano, Julai 16, 2025, yakilenga jengo la Jeshi, Wizara ya Ulinzi na maeneo jirani ya Kasri la Rais. Mashambulizi ya awali yalikuwa yamepiga maeneo mengi viungani mwa Damascus, Daraa na Sweida, yakilenga maeneo ya kijeshi na misafara ya jeshi la Syria na vikosi jumla vya usalama vilivyokuwa vikielekea Sweida, na kusababisha idadi kubwa ya mashahidi na majeruhi.

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu