Jumapili, 25 Muharram 1447 | 2025/07/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran na Athari zake

Al Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 27/6/2025: "Vyanzo vinne vyenye taaarifa vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kufikia hadi dolari bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya kiraia. Vyanzo hivyo viliongeza kuwa majadiliano haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kwamba mapendekezo kadhaa yamewsilishwa, ya awali pamoja na yaliyoboreshwa, yakiwa na kifungu kimoja kisichobadilika, kisichoweza kujadiliwa : “kukomeshwa kabisa kwa urutubishaji wa urania ya Iran.”

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama katika Mji wa Al-Qadarif Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir vikiliunga mkono umbile la Kiyahudi!

Katika hotuba ya hadhara iliyotolewa na Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Qadarif, kwenye soko la Al-Qadarif karibu na hospitali ya meno, mnamo siku ya Alhamisi, tarehe 23 Dhul-Hijjah 1446 H, inayolingana na 19/6/2025 M, Ustadh Awad Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza kuhusu uhalisia wa vita na umbile la Kiyahudi, furaha ya Waislamu kwa mashambulizi dhidi ya umbile hili, na kiu ya watu ya ushindi dhidi ya mkaaji huyu wa kimabavu wa ardhi tukufu—Masrah ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Alithibitisha faradhi ya kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo itaikomboa Palestina na ardhi nyenginezo za Kiislamu zinazokaliwa kwa mabavu. Hadhira iliitikia vyema hotuba hiyo, na kulikuwa na michangio tofauti tofauti kutoka kwa waliohudhuria.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Matembezi yaliyohudhuriwa na umati mkubwa wa watu yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia yalitoka katika mji mkuu wa Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, mnamo tarehe 20 Juni 2025 M kuanzia Msikiti wa Al-Fath chini ya kichwa: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Soma zaidi...

Ni Dhambi Kubwa Kwa Ndege za Mayahudi Kuvuka Anga ya Tawala, Kuipiga Mabomu Iran na Kurudi Salama Bila Kutunguliwa na Tawala hizi Hata kwa Risasi Moja!

Trump alisema katika chapisho kwenye jukwaa la Kijamii la ‘Truth’: ["Iran na Israel wanapaswa kufanya makubaliano, na watafanya makubaliano, kama vile nilivyozifanya India na Pakistan kufanya." Aliendelea: "Vivyo hivyo, tutakuwa na AMANI, hivi karibuni, kati ya Israel na Iran! Miito mingi na mikutano inafanyika hivi sasa."(Sky News,15/6/2025). Mnamo Jumapili, msemaji wa jeshi la umbile la Kiyahudi alisema kupitia jukwaa la X kwamba "Israel ilitoa onyo kwa Wairan wanaoishi karibu na vinu vya nyuklia nchini Iran kuhama makaazi yao." Wakati huo huo, msemaji wa jeshi la 'Israel' alisema kuwa jeshi lilishambulia kituo cha nyuklia katika mji wa Isfahan, katikati mwa Iran. Tangu alfajiri ya Jumapili, Iran ilianza kurusha raundi mpya za makombora kwenye shabaha ndani ya 'Israel', na kusababisha vifo na makumi ya majeruhi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa nyumba na majengo. Kwa kujibu, Tehran imekuwa chini ya mashambulizi ya 'Israeli'. (Al Jazeera,15/6/2025).

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu