Alhamisi, 08 Muharram 1447 | 2025/07/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  2 Muharram 1447 Na: 1447 / 01
M.  Ijumaa, 27 Juni 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Kuna Tofauti Kubwa kati ya Utu chini ya Uislamu na Udhalilifu chini ya Ukandamizaji wa Tawala za Kitumwa
(Imetafsiriwa)

Kamati ya Kuu ya Mitihani ya Cheti cha Sudan ilitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na mashirika husika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu na kusaidia kuwawezesha wanafunzi wote wa Sudan kufanya mitihani, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na vita na hali ngumu ya kibinadamu. (SUNA, Juni 26, 2025)

Kundi la wananchi wenzetu bado wana matumaini mema katika Umoja wa Mataifa na mashirika yake, na wanatumai kupata msaada kutoka kwa wale wanaoitwa jumuiya ya kimataifa na mashirika ya kimataifa, licha ya historia yao, ambayo inathibitisha kuwa hawatoi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Sio mashirika ya kutoa misaada, bali yana ajenda inayodhihirisha uadui wake wa wazi dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Mnamo mwaka wa 2016, UNESCO ilifanya kongamano kuhusu kuzuia misimamo mikali yenye vurugu, ambalo lilihitimisha kwamba “suala la kubadilisha mitaala ya elimu katika Mashariki ya Kati na maeneo mengine ambako fikra za msimamo mkali zinashamiri lazima lishughulikiwe.”

Neno hili, "itikadi kali," linatumika kwa kumaanisha Uislamu pekee. Kwa sababu dola za Magharibi zinazotawala ulimwengu wa leo zinataka Uislamu wa kikuhani usio na uhusiano wowote na maisha ya kila siku, iwe katika masuala ya utawala, siasa, uchumi, au mifumo ya kijamii, zinataka kuepuka vikwazo vyovyote katika mipango yao. Hakika wanaendelea na vitendo vyao vyote vya uhalifu dhidi ya Waislamu, yakiwemo mateso na mauaji ya halaiki. Kujitenga kwa Sudan Kusini na vita vinavyoendelea hivi sasa nchini Sudan si chochote ila ni matokeo ya kufuata nchi za Magharibi za kibepari na mashirika yake ya uhalifu.

Dori ya mashirika haya yanayoitwa ya kibinadamu ni zaidi ya kile kinachotangazwa, kujaribu kupotosha rai jumla kwa kusambaza habari za kupotosha kuhusu hali ya kweli katika maeneo ambayo wanafanya kazi, ili kuendelea na kazi yao. Hii ni pamoja na dori zao za kijasusi zenye kutia shaka kwa niaba ya dola za kimataifa, kiasi kwamba wachunguzi kadhaa wamezitaja kuwa ni ala za ukoloni mamboleo! Hakika, ni miongoni mwa ala hatari zaidi za mizozo wa kimataifa.

Nchini Sudan, ni mara ngapi mashirika haya ya kimataifa yamefichuliwa kwa kufanya kazi za kiuchunguzi na kijasusi kwa nchi za Magharibi? Hii haiishii katika kukusanya habari tu, bali inaenea hadi kupanda sumu ya mgawanyiko na migogoro kati ya makundi ya watu, kama ilivyotokea huko Sudan Kusini, ambapo mashirika haya, kwa kuchukua upande mmoja katika mzozo, yalichangia utata wa migogoro hii, kwa kutumia kinga iliyotolewa kwao.

Kusimamia masuala kunahitaji kuamiliana na mashirika haya ya kimataifa kwa kutokuwa na imani nayo. Matendo yao, ambayo yamezua shaka nyingi, yana sifa ya sintofahamu kubwa kutokana na maslahi yanayokinzana na misimamo isiyoeleweka ya nchi zinazoyasaidia.

Wokovu wetu uko mikononi mwetu wenyewe, si mikononi mwa adui zetu wanaotuvizia, iwe ni wale wanaotutangazia uadui wao waziwazi au wale wanaovaa kwa unafiki vazi la marafiki na vazi la “washirika” (wafadhili). Kunasibisha masuala ya elimu, ambayo ni muhimu zaidi katika kuinua na kuunda vizazi, na mashirika haya yenye shaka ni kujiua kisiasa na maafa makubwa, madhara ambayo yataonekana wazi kwa jamii hivi karibuni.

Elimu ni nguzo msingi ya mwamko wa Waislamu. Ili kufikia hili, mfumo wa kisiasa unaoegemezwa kwenye imani kubwa ya Uislamu ni muhimu. Mfumo unaojumuisha ruwaza ya kipekee, iliyoinuliwa na huru ya kisiasa kwa dola yake, inayomwongoza mwanadamu kutoka kwenye giza la ukafiri, upotofu, na ujinga hadi kwenye nuru na uadilifu wa Uislamu, ambao inauleta kwa wanadamu katika nyanja zote za maisha: kiroho, kifikra, kimaadili, kisiasa, kiuchumi, na zaidi ya hayo, na pia katika sayansi na teknolojia. Mfumo huu wa kisiasa, kwa ufupi, ni Khilafah Rashida, kwa njia ya Utume, ambayo inatekeleza kikamilifu Uislamu na mifumo yake. Imeongoza ulimwengu kwa karne nyingi katika ubora wa taasisi zake za kitaaluma, uvumbuzi na ugunduzi wake wa hali ya juu, pamoja na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya mwanadamu. Kuna tofauti kubwa kati ya utu chini ya Uislamu na udhalilifu chini ya mifumo ya utumwa.

Msemaji Rasmi wa Kike wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 0912240143- 0912377707
http://www.hizb-sudan.org/
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com
Yaliyomo ndani ya kifungu hichi: « Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu