Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan - mbele ya Msikiti Mkuu jijini Port Sudan Wito kwa Watu wa Sudan... Msiiruhusu Amerika Kuichana Nchi Yenu na Kuivua Darfur
- Imepeperushwa katika Sudan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi Waislamu: Mataifa katika maisha yao yana masuala nyeti, yaani, masuala ambayo mtu anakuwa na msimamo mmoja: yhai chini yao au kifo kwao. Itikadi ya Uislamu imetubainishia sisi Waislamu masuala yetu nyeti; yaani yale ambayo kipimo chake ni uhai au kifo. Miongoni mwa masuala hayo nyeti ni suala la umoja wa dola na umoja wa Ummah. Tulipoondoa suala hili kwenye kituo chake stahiki hapo awali, Amerika, kwa msaada wa baadhi ya watu wetu, iliweza kuichana nchi yetu na kuitenganisha Sudan Kusini, na sasa inaregea kukamilisha kile ilichoanza mwanzo kuchora, kwa mipaka ya damu, dola mpya katika mabaki ya nchi yetu; kwa kuivua Darfur, ambako matukio yanazidi kupamba moto katika kutumikia njama ya Amerika kwa usaidizi wa zana zake ndani na nje.



