Jumamosi, 18 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

Jana, Jumatatu, tarehe 8/9/2025, huko Rabak, mji mkuu wa Jimbo la White Nile, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ulikutana na Sheikh Abdullah Al-Nur Tutu, Imam na Khatib wa Msikiti Mkuu wa Asalaya na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni wa Sudan, Tawi la White Nile, nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo uliongozwa na wafuatao Dkt. Ahmad Mohammad, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Faisal Madani, Abdul Majeed Osman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Ndani ya Muundo wa Kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kuvuruga Mpango wa Kutenganisha Darfur Wanachama wa Hizb ut Tahrir katika Mji wa Al-Obeid Wahutubia Wito Mzito kwa Waislamu katika Msikiti Mkuu wa Al-Obeid na Kubeba Mabango katika Amali Ny

Katika amali mbili tofauti, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumamosi tarehe 06/09/2025, na ndani ya muundo wa kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ya kuvuruga mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Umma ni suala nyeti ambalo kwalo kipimo ni uha na kifo.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nadir Muhammad Hussein, mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, wanachama wa Hizb ut Tahrir, walimtembelea Ustadh Al-Tijani Abdul Wahab, mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan, nyumbani kwake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Ijumaa tarehe 05/09/2025, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Matendo ya Watawala wa Sudan na Misri Kuhusu Bwawa la An-Nahdha Upotevu wa Usalama wa Maji kwa Watu wa Bonde la Nile

Utaratibu wa mashauriano baina ya nchi mbili unaojulikana kama 2+2, unaojumuisha mawaziri wa mambo ya nje na unyunyiziaji maji wa Misri na Sudan, walifanya mkutano katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri mnamo Jumatano, 3/9/2025, kujadili maendeleo katika faili la Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD). Mkutano huo ulisababisha taarifa ya pamoja ambapo pande hizo mbili zilieleza makubaliano yao kamili kuhusu hatari ya hatua za upande mmoja zinazochukuliwa na Ethiopia kuhusu ujazaji na uendeshaji wa bwawa la GERD. Taarifa hiyo iliashiria hatari kadhaa zinazohusishwa na bwawa hilo, ikiwa ni pamoja na dhamana dhaifu ya usalama, mtiririko wa maji usio wa kawaida, na athari zinazoweza kutokea wakati wa ukame.

Soma zaidi...

Maslahi ya Nani Yanatumikiwa kwa Uamuzi wa Serikali wa Kufungua Tena Kivuko cha Mpakani cha Adre huku Watu wa Fashir Wakifa kwa Njaa?!

Serikali ya Sudan ilitangaza mnamo Jumanne kwamba itaongeza muda wa ufunguzi wa kivuko cha mpakani na Chad cha Adre kwa mashirika ya misaada ya kibinadamu hadi mwisho wa mwaka huu. Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa taarifa ikisema kwamba hatua hii inathibitisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kwamba misaada ya kibinadamu inawafikia wale wanaohitaji nchini kote, na kuonyesha nia yake njema katika kuwezesha shughuli za kibinadamu.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Mnaweza Kutibua Mpango wa Kuitenga Darfur, Basi Inukeni Kumtii Mwenyezi Mungu!

Katika hatua inayotarajiwa, kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo, alikula kiapo cha kikatiba kama mkuu wa Baraza la Rais la kile kinachoitwa serikali sambamba huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, mnamo Jumamosi, 30/8/2025. Makamu wa Rais, wajumbe wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu pia walikula kiapo.

Soma zaidi...

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na vita kati ya pande zinazopigana, ambapo makumi ya raia waliuawa katika siku chache zilizopita, huku wakaazi wakiteseka kutokana na kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, katika kivuli cha kimya cha kituliwa shaka cha kimataifa, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha mauaji ya angalau watu 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu