Jumapili, 22 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan – Mji wa Rabak, White Nile, uliitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri mnamo Jumapili, 1 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 24 Agosti 2025. Ujumbe huo ulikutana na mkuu wa Sekretarieti katika Jimbo la White Nile, Sheikh Abdul Mubara Mahmoud Al-Mahmoud. Ujumbe huo uliongozwa na Dkt. Ahmed Muhammad Fadl Al-Sayyid, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na alifuatana na Ustadh Faisal Madani, mwanachama wa Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika ndugu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Hatim Jaafar, mwanasheria - mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi, 22 Safar 1447 H sawia na 16/08/2025 M, yenye kichwa: “Wito kwa Watu wa Sudan... Ikamateni Darfur Ili Isiungane na Kusini”

Mnamo Jumamosi, 26/7/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilitangaza kuundwa kwa serikali sambamba na serikali iliyopo nchini Sudan, katika mji mkuu wa Darfur Kusini (Nyala). Hatua hii ya RSF ni hatua ya juu katika kutenganisha eneo la Darfur, ambalo inalidhibiti, isipokuwa sehemu za mji wa El Fasher, ambao mzingiro wa kukandamiza umewekwa juu yake kwa zaidi ya mwaka mmoja, na kuanzisha mashambulizi mfululizo dhidi yake ili kuuangusha, ili eneo zima la Darfur liwe chini ya udhibiti wake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tuna furaha kuwaalika ndugu zetu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na mambo ya umma kuhudhuria kwenye mkutano na waandishi wa habari, ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan atatoa hotuba kwa anwani: "Wito kwa Watu wa Sudan: Ikamateni Darfur ili Isijiunge na Kusin"

Soma zaidi...

Mbwa Mwitu Hapaswi Kulaumiwa kwa Uvamizi wake ikiwa Mchungaji ndiye Adui wa Kondoo

Watoto watatu walifariki katika Jimbo la Khartoum baada ya kupokea dozi ya chanjo ya ukambi. Wizara ya Afya imefungua uchunguzi kuhusu dhurufu za vifo vyao. Sudan Tribune iligundua kuwa watoto wawili walikufa ndani ya saa moja baada ya kupokea chanjo ya ukambi, huku mtoto wa tatu akifa siku tisa baada ya kusaidiwa kupumua katika Hospitali ya Al-Balak mjini Omdurman. (Sudan Tribune, Agosti 5, 2025)

Soma zaidi...

Mahusiano ya Kigeni ni Jukumu la Dola Pekee, kwa kuwa Dola Pekee ndiyo iliyo na Haki ya Kuchunga Mambo ya Ummah Kivitendo

Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wajumbe kutoka Muungano wa Vyama na Mavuguvugu ya Sudan Mashariki, wakiongozwa na Sheiba Dirar na kuandamana na kundi la watu mashuhuri, walikutana na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki mnamo Jumamosi, 2 Agosti 2025, afisini kwake huko Adi Halo, ambapo wajumbe hao walijadiliana naye hali ya sasa ya Sudan kwa jumla, kwa kuzingatia changamoto zinazoikabili Sudan Mashariki. Ujumbe huo pia ulisisitiza umuhimu wa uratibu na nchi jirani ili kusaidia utulivu wa nchi na kukabiliana na migogoro ya kisiasa na usalama.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Hotuba Iliyotolewa na Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan mnamo Ijumaa tarehe 1/8/2025 M

Je, hili linaweza kuwaziwa kutoka kwenu?! Vipi mnaweza kula, kunywa na kulala na hali ndugu zenu mjini Gaza wanauawa, wanahamishwa na kuwekwa njaa na Mayahudi wanaokalia kimabavu eneo la Isra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)?! Dhambi liko juu ya shingo zetu sote ikiwa hatutawanusuru ndugu na dada zetu wa Gaza. Hatutaweza kuwanusuru isipokuwa majeshi ya Umma yasonge, kwani wao ni watoto wenu na ndugu zenu, na hakuna kitakachowaondoa Mayahudi isipokuwa dola ya Waislamu; Khilafah.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu