Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Jibu la Swali

Ukweli wa Mgogoro wa Ukraine, Vipimo na Malengo Yake

(Imetafsiriwa)

Swali:

Mnamo tarehe 20/12/2021, Al-Jazeera ilichapisha kwenye tovuti yake: “Jeshi la Ukraine na watu wanaotaka kujitenga wanaoungwa mkono na Moscow walikabiliana kwa risasi, na kusababisha vifo katika pande zote mbili... Matukio haya yanakuja siku moja baada ya Katibu wa Usalama wa Taifa na Baraza la Ulinzi la Ukraine Alexey Danilov kutangaza kuwa nchi yake, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi, iliandaa mpango wa kina wa utekelezaji, ambapo mashirika yote na sekta za jeshi zitashiriki, kwa kutarajia uvamizi wowote wa Urusi, kama alivyosema. Ukraine ilikuwa imeishutumu Urusi kwa kukusanya hadi wanajeshi 100,000 karibu na mipaka yake ili kujitayarisha kuishambulia ifikapo mwisho wa Januari ijayo... Hata hivyo, Urusi ilikanusha kuwa inapanga kuivamia Ukraine...” [Al Jazeera 20/12/2021 ] Je, ukweli wa mgogoro huu ni upi na vipimo na malengo yake? Je, ni nini kinachotarajiwa kwa mkolezo huu, haswa wa Urusi-Marekani?

Jibu:

Ili kupata jibu wazi, tunahakiki mambo yafuatayo

1- Urusi ya ki-Tsar ilichukua udhibiti wa eneo la Ukraine wakati wa karne ya kumi na sita, kisha watu wa Ukraine walishiriki katika ukoloni wa Urusi wa maeneo mengine yote na kuwawezesha kuwakoloni watu wengine. Kwa kiwango ambacho watu wa ukoloni hawakutofautisha kati ya Warusi na Waukraine, haswa kwamba wote wawili walikuwa Wa-Slavic. Muungano wa Kisovieti uliposambaratika mwaka wa 1991, Ukraine ilipata uhuru wake mwaka wa 1991. Ikawa nchi ya pili katika nafasi ya Muungano wa Sovieti, yenye eneo la pekee kaskazini mwa Bahari Nyeusi, ikiwa na idadi kubwa ya watu milioni 40 yenye muundo wa kiviwanda usio chini ya ule wa Urusi, na silaha za nyuklia zinazowakilisha theluthi moja ya urithi wa Soviet, kabla ya kupokonywa na makubaliano ya Amerika-Urusi na Ukraine kwa ahadi ya Amerika-Urusi ya kuhifadhi uhuru wa Ukraine. Ukraine imeshiriki katika mazungumzo marefu na magumu na Urusi kuhusu Meli za Bahari Nyeusi ya Soviet, ambazo nyingi zake Urusi ilirithi na ziko katika bandari ya Sevastopol huko Crimea ndani ya Ukraine chini ya makubaliano ya kukodisha.

2- Nguvu ya Urusi ilishindwa kuirejesha Ukraine mikononi mwake katika kila mzozo na Ukraine, iwe ni wakati wa suala la kugawanya Meli za Bahari Nyeusi mwanzoni mwa miaka ya tisini, au mabomba marefu na mapana ya gesi ambayo Umoja wa Kisovieti ulijenga ndani ya Ukraine kusafirisha gesi kutoka eneo la Urusi hadi Ulaya. Ni nini kiliibuka baada ya suala hili la hitaji la Urusi kwa njia mbadala kama vile Mkondo wa Kituruki kupitia Bahari Nyeusi au Mkondo wa Kaskazini kupitia Bahari ya Baltic hadi Ujerumani, au katika maswala ya kibiashara ambapo soko la Urusi linahitaji sana sukari na mafuta yanayozalishwa na ardhi yenye rutuba ya Ukraine, au suala la uanachama wa Ukraine katika vyombo mbalimbali vilivyoanzishwa na Urusi kwa ajili ya nchi za mfumo wa zamani wa Usovieti, au baada ya hapo kuibuka kwa mielekeo ya Kiukreni kuelekea Umoja wa Ulaya na NATO, migogoro yote hii ya Urusi na Ukraine haikuiwezesha Urusi kuitawala tena Ukraine katika miongo mitatu iliyopita licha ya ukuu wa kijeshi wa Urusi.

3- Ukraine ni uwanja wa mbele wa Urusi. Urusi sio kama Asia ya Kati, kwa mfano, kama uwanja wa nyuma katika suala la eneo, mafungamano ya kitaifa ya kidini na kihistoria. Inapuuza Bahari Nyeusi na kuidhibiti juu ya mtazamo wake kutoka kwa maeneo ya Kiislamu ya Caucasian ambayo Urusi imeyakalia katika kipindi chote cha kihistoria. Kutoka ardhi yenye rutuba ya Ukraine, Urusi inapata uhakika wake wa chakula katika bidhaa za kimsingi zinazoilinda kutokana na mabadiliko ya mahusiano yake na nchi za Magharibi, ambako inavuka hadi Ulaya Mashariki, iwe kwa mabomba ya gesi au vinginevyo. Zaidi ya yote, Ukraine leo inawakilisha eneo la mwisho la ngome ya  kutatua utata wa kihistoria wa Urusi, ambayo ni hofu ya Uropa ambayo ilivamiwa mara mbili (Napoleon na Hitler), na ikiwa udhaifu wa serikali ya Soviet ulilazimisha kuachana na Ulaya Mashariki kama eneo la ngome, katika kukabiliana na maendeleo ya NATO kuelekea Ulaya Mashariki, angalau inataka majirani zake Ukraine na Belarusi kuipatia eneo ambalo linaitenga na hatari za NATO na maendeleo ya mikakati  yake ya kijeshi kuelekea mashariki. Urusi leo inataka kuizuia Ukraine kujiunga na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO), au kuiunga mkono [na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergey Ryabkov aliona uungaji mkono wa kijeshi wa Marekani kwa Ukraine kuwa "changamoto kubwa kwa usalama wa Urusi." (Al-Ain Al-Ikhbarya, 13/4/2021)].

4- Nchi za Magharibi, hasa Marekani, zilitambua ukweli wa utata huu wa Ukraine katika siasa za Urusi, na kwamba Ukraine inawakilisha upande dhaifu wa Urusi, hasa baada ya kuzuka upya kwa vuguvugu la utaifa nchini Ukraine kuzidi na uadui wake dhidi ya Urusi kukita mizizi. Kwa hiyo, Ukraine ikawa, kwa miongo miwili, kituo cha msuguano wa Marekani na Ulaya na Urusi. Kufuatia Mapinduzi ya Orange yaliyompindua Rais wa Ukraine Yanukovych mwaka 2014, Moscow ilijibu katika mwaka huo huo kwa kukata Peninsula ya Crimea kusini kutoka Ukraine na kuiunganisha kwa Urusi, ambayo ina kambi za kimkakati na kubwa za kijeshi katika kisiwa hicho. Haikuridhika na hilo, lakini iliwasukuma Warusi wanaotaka kujitenga huko Ukraine kuwasha moto mikoa ya mashariki na kutangaza uhuru wa majimbo mawili (Donetsk na Luhansk) kuitwa na Warusi kama "Urusi Ndogo", na kutoa msaada wa kijeshi kwake. Haya yote yaliisukuma Ukraine katika mikono ya nchi za Magharibi. Baada ya hapo Ukraine ilidai na kusisitiza kujiunga na NATO kwa matumaini kwamba ingeilinda dhidi ya uvamizi wa Urusi. Wamagharibi walianza kuisogeza karibu, wakionekana kama mlinzi wake. Ukraine ilianza kualikwa kwenye mikutano ya Uropa na NATO, haswa wakati machafuko na Urusi yalipozidi bila kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Ulaya au NATO. Marekani ilianza kuipatia silaha na kuipatia mabilioni ya dolari katika msaada wa kijeshi, na ilianza kutoa mafunzo kwa jeshi lake.

5- Urusi imekuwa chini ya vikwazo vikali vya nchi za Magharibi (Ulaya na Marekani) tangu ilipotwaa Crimea, hivyo ilijaribu kufidia kwa kuongeza mahusiano yake ya kiuchumi na China. Ilipanua mabomba hadi China kusafirisha mafuta na gesi, na kuifungulia China njia ya ardhini (reli) kusafirisha bidhaa za China moja kwa moja hadi Ulaya, yaani, ilishirikiana nayo katika mfumo wa mradi mkubwa wa China wa "Silk Road", na kuendelea. Juu ya hayo, ilianza kuondoa hisa zake za bondi na dolari za Marekani na kwa kiasi kikubwa ikaachilia biashara yake ya dolari. Ingawa Urusi haina uwezo mkubwa wa kibiashara kama Ulaya au Uchina, Marekani iliona kwamba Urusi inapinga utawala wa kiuchumi wa Marekani na kwa ujasiri inachochea nchi nyingine kufanya hivyo. Hili linadhihirika katika mikataba mingi ya kibiashara ya Urusi, hasa na Uchina, kwa kupitisha sarafu za ndani badala ya dolari. Hili lilikuwa tishio kwa Marekani, na kuongeza kwake tuhuma ya hivi karibuni kwamba Urusi inaongeza bei ya gesi, kuwa shida mpya ya kiuchumi kwa Uropa.

6- Urusi inazingatia vipimo na faida kubwa za Ukraine katika historia, ufalme, uchumi na usalama, yaani, eneo la ngome kutoka NATO, na kwa hivyo inachukulia kuwa mstari mwekundu, (Putin aliionya NATO dhidi ya kupeleka vikosi na silaha zake huko Ukraine, akisema: “Kupanua miundombinu ya kijeshi ya NATO nchini Ukraine” ni mstari mwekundu kwa Urusi na itachochea jibu kali.” Hata hivyo, Rais wa Marekani Joe Biden alisema kwamba haheshimu mistari yoyote myekundu kuhusu Ukraine. (Noon Post, 4/12/2021), kwa yote hayo, wakati inasimamia mzozo wa sasa wa Ukraine, Urusi haiko karibu kuiacha Ukraine na kuiacha kuwa mawindo rahisi kwa Marekani na NATO, haswa baada ya kujaribu na kuvumilia vikwazo vya Magharibi, na zaidi kwamba, inaamini kwamba wasiwasi mkuu wa Marekani leo ni kuikabili China, ikimaanisha kuwa Marekani haitaifanya Ukraine kuwa mwanachama wa NATO kwa sababu ya rasilimali muhimu za Marekani kuilinda Ukraine; kwani hii itadhoofisha maandalizi ya Marekani katika Mashariki ya Mbali kukabiliana na China... Kama vile Urusi haithamini Ulaya, ambayo haina nguvu za kijeshi na inategemea Urusi kwa kiwango kikubwa katika masuala ya usambazaji wa nishati, ikimaanisha kuwa Urusi inahisi kuwa hali ya kimataifa ni nzuri kwake kupata mafanikio Ukraine. Kwa hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov alimwambia mwenzake wa Marekani, Anthony Blinken, kwamba Moscow inahitaji (dhamana ya usalama ya muda mrefu katika mipaka yake ya magharibi ambayo ingezuia upanuzi wa Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini - NATO - mashariki ... na kuongeza," ambalo lazima lichukuliwe kuwa hitaji la lazima"), kama ilivyonukuliwa na Bawabat Al-Wasat ya Libya mnamo 2/12/2021.

7- Huu ndio ukweli wa madai kutoka kwa upande wa Urusi ambao unasimama nyuma ya mzozo huu wa Ukraine. Urusi inaamini kuwa nchi za Magharibi zinaongeza silaha zake nchini Ukraine, na kwamba nchi za Magharibi zinaweza kuisukuma Ukraine baada ya kuimarisha jeshi lake ili kuwatokomeza waasi wa Urusi walioko mashariki mwa Ukraine, na kisha kuisukuma kwenye vita huko Crimea. Na haya yote ni hatari kwa Urusi, Mkuu wa Majeshi wa Urusi, Valery Gerasimov, alisema: [Ugavi wa ndege, droni na helikopta kwa Ukraine utaisukuma Kiev kuchukua hatua za hatari... Lakini chokochoko zozote za Kiev kutatua hali nchini Donbass zitazimwa kwa nguvu. (RT, 9/12/2021)]. Kwa hivyo, mzozo wa sasa unaonyesha kuwa Urusi inalenga kwanza kutotilia shaka kwamba Crimea ni sehemu yake, lakini inataka hilo kama chambo kutambuliwa kimataifa na Marekani na Ulaya. Lengo la pili ni Mashariki ya Ukraine kuwa nje ya mamlaka ya Ukraine na sehemu ya Urusi, na lengo la tatu lenye ufanisi zaidi ni kuizuia Ukraine isijiunge na NATO na inahitaji dhamana kwa hilo, hasa baada ya mazoezi ya pamoja ya kijeshi kati ya NATO na Ukraine katika Bahari Nyeusi, ambapo Rais wa Urusi Vladimir Putin alisema wakati huo (kwamba mazoezi ya hivi karibuni yaliyofanywa na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) katika Bahari Nyeusi yalizidi mipaka yote, na kuona kwamba Magharibi haichukui maonyo ya nchi yake kwa uzito wa kutosha. Katika hotuba yake kwa maafisa wa sera za kigeni mjini Moscow, Rais wa Urusi alionyesha kuwa safari ya ndege ya washambuliaji wa kimkakati wa NATO umbali wa kilomita 20 kutoka kwenye mipaka ya nchi yake inavuka mipaka yote inayokubalika. Alisema “Washirika wetu wa Magharib wanazidi kuharibu hali kwa kuipatia silaha Kiev na kuendesha mazoezi ya kijeshi yenye uchochezi.” (Al-Jazeera Net, 18/11/2021)

8- Marekani ilijibu madai ya Urusi kwa kufanya mkutano kati ya Rais wa Urusi Putin na Biden wa Marekani. Mkutano huo ulifanyika tarehe 7/12/2021, na mgogoro wa Ukraine ulikuwa mada yake kuu, lakini haikuwa pekee. Wakati wa mkutano huo, ilionekana kuwa Urusi inaitaka Marekani kutambua mistari myekundu inayochora nchini Ukraine. Pia iliibuka kuwa Marekani inaionya Urusi juu ya vikwazo vya kiuchumi ikiwa itaivamia Ukraine, na Marekani haina chochote zaidi ya hayo. Rais wa Marekani alithibitisha siku moja baada ya mkutano huo kwamba uingiliaji wa kijeshi wa Marekani katika tukio la uvamizi wa Urusi nchini Ukraine sio chaguo, na Marekani ilitishia kabla ya mkutano huo na kwa maneno ya viongozi wengi kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo haijawahi kushuhudia tangu hapo, na ilizungumza juu ya kuzuia mtiririko wa gesi ya Urusi kwenye laini ya mkondo wa Kaskazini hadi Ujerumani, na kwamba inazungumza na Wajerumani katika suala hili. Kinachoweza kufanywa zaidi ni kuiondoa Urusi na benki yake kuu kutoka kwa mfumo wa kutuma pesa kutoka nje, ingawa biashara nyingi za Urusi hazitumii dolari.

9- Kwa kuchunguza suala hilo, tunaona kwamba Urusi inajiingiza kwenye mgogoro ambao inaweza kujirudi yenyewe. Marekani inaweza kumshinikiza rais wa Ukraine kuichokoza Urusi ili Urusi isiwe na nafasi wala chaguo ila kuivamia Ukraine, ikwame kwenye matope ya Ukraine na kuingia matatani na Ulaya. Ukraine sio nchi mwanachama wa NATO kwa Marekani kujitetea. Iwapo Urusi itafanya makosa na kuivamia Ukraine, itaipatia Marekani sababu zote za kuziitiisha nchi za Ulaya na kuzirudisha chini ya vazi la Marekani kwa kisingizio cha kusimama katika mstari dhidi ya uchokozi wa Urusi, ambao hauendani na msururu wa siasa za kimataifa unaotetewa na Urusi. Pia kuna upande ambao Urusi haioni. Ikiwa ni shinikizo la Marekani kwa Urusi katika tukio la uvamizi wake nchini Ukraine, Marekani itakuwa na chombo kipya cha kusambaratisha muungano unaoibukia kati ya Urusi na China. Inaweza kuweka shinikizo kwa China na kuitishia kupitia biashara yake na Marekani ili kujiweka mbali na Urusi inayoishambulia Ukraine: Ikiwa China itajisalimisha na kujiweka mbali na Urusi, basi Marekani itakuwa imefikia lengo kubwa, na ikiwa Urusi itajisalimisha kwa aina mbalimbali za vikwazo na kujiondoa kutoka Ukraine baada ya uvamizi wake, matakwa ya Marekani yataifuata mashariki mwa Ukraine, na hata huko Crimea, kuinyima Urusi faida yoyote kutokana na uvamizi wake wa Ukraine, badala yake itaipeleka kwenye majanga, hii ni pamoja na Marekani kuzichochea nchi za Ulaya Mashariki na kuzifanya zitoe msaada wa kijeshi wenye nguvu na madhubuti kushambulia Urusi huko Ukraine, na labda matukio ya uchovu wa Urusi huko Afghanistan hayako mbali kukumbukika. Kwa haya yote, Urusi inacheza mchezo hatari karibu na Ukraine ambao unaweza kuwa mtego mkubwa kwake na kugeuka dhidi yake, yaani, kama mpumbavu ambaye hatambui matokeo ya hatua yake.

10- Kuhusu wapi mambo yanaelekea, jawabu ni kama ifuatavyo.

a- Nchi za Ulaya zinataka kutuliza hali na kuzuia Urusi kuivamia Ukraine, na zinataka kulainisha uhusiano na Urusi ili kupunguza hatari zake na kuhakikisha utiririshaji wa rasilimali za nishati ya Urusi kwenda Ulaya kwa bei nzuri. Ufaransa, Ujerumani na Italia zinatoa wito kwa Urusi kufanya mazungumzo na Ukraine ili kutatua mgogoro huo, ikiwa ni pamoja na (Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Heiko Maas aliyesema kuwa nchi yake inataka kuboresha uhusiano na Urusi. Waziri huyo alisisitiza kuwa ili kufikia hilo kunahitaji maendeleo katika kutatua mzozo huo nchini humo Donbass.(RT, 23/11/2021), lakini Uingereza inaweza kutaka kuzidisha mvutano huo kutokana na upinzani wa kisiasa kwa Umoja wa Ulaya, ambao ilijiondoa! [Mkuu wa Majeshi ya Uingereza, Jenerali Nicholas Carter, alisema kuna hatari kuliko wakati wowote ule tangu Vita Baridi, vya kati ya Magharibi na Urusi. (Al Jazeera Net, 13/11/2021)], na zaidi akasema, [“Tunapaswa kuwa waangalifu” kuhusu uwezekano wa kuzuka kwa mlipuko wa mizozo katika eneo hilo. Jenerali Nick Carter aliambia BBC kwamba anatumai kwamba kikweli hakutakuwa na vita na Urusi, lakini akaongeza kuwa NATO inapaswa kuwa tayari kwa uwezekano huu.(BBC, 5/12/2021)], na taarifa kama hizo kutoka Uingereza zinapaswa kuzua mtafaruku zaidi ya kuwa vielezo vya vita halisi.

b- Lakini jambo la kuamua zaidi ni msimamo wa Marekani, kwani inadhibiti nyuzi nyingi za serikali ya Ukraine, na kwa sababu hiyo Urusi ilituma barua ya kuomba dhamana ya usalama, ambayo iliituma Marekani na sio nchi nyingine yoyote kwa msingi kwamba nchi za muungano huo zinafuata hatua zake, hata kama Marekani ilichelewa kujibu kuhusu dhamana ya usalama, hasa suala la kujiunga kwa Ukraine katika muungano, ucheleweshaji huu unatia wasiwasi: [“Huko Moscow, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergey Ryabkov alisema kwamba Moscow inahitaji majibu ya haraka ya Marekani kwa mapendekezo yake kwa sababu hali ni ngumu na inakabiliwa na matatizo na hata kuongezeka.” (Al Jazeera, 20/12/2021)], na kadhalika.

- Ikiwa Marekani itaamua kuipa Urusi dhamana ya usalama nchini Ukraine bila kukubaliana nayo juu ya Uchina, basi upande wa Urusi utakuwa mkubwa katika mzozo huu. Kutoa dhamana hizi kunadhihirisha udhaifu zaidi wa msimamo wa Marekani kwa sababu Marekani ingekubali matakwa ya Urusi na kusikiliza matakwa ya Ulaya ili kurahisisha hali hiyo, na hilo haliwezekani isipokuwa iwapo makubaliano ya Urusi yatafanyika, kuvunja uhusiano wake na China kwa maslahi ya nchi ya Marekani.

- Lakini ikiwa Marekani itaamua kuihusisha Urusi na kuisukuma vitani nchini Ukraine, basi Urusi itakuwa imeanguka au kunaswa katika mpango wake.

- Kwa kutafakari mambo haya, kuna uwezekano mkubwa kwamba vita vikali kati ya Urusi na Ukraine havitarajiwi kutokea isipokuwa maendeleo mapya yatatokea, ambayo Urusi inadanganywa, na vita huanza na kuhusika ndani yake! Kutokuwa na matarajio ya vita hakuzuii mapigano ya hapa na pale mashariki mwa Ukraine...

Kadhalika, haitarajiwi kwamba Marekani itapata kukata kabisa uhusiano wa Urusi na China... Kwa upande wake, Urusi haitafikia malengo yake matatu... Badala yake, inawezekana, na kwa maelewano ya mabepari, kwamba Marekani italainisha misimamo yake kuelekea malengo matatu ya Urusi kwa kubadilishana na Urusi kurahisisha uhusiano wake na China... Na kisha Urusi iondoe jeshi lake kwenye mpaka wa Ukraine, na kuondoka mikono mitupu!

18 Jumada al-Awwal 1443 H

22/12/2021 M

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu