Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Silsila ya Maswali Yaliyowasilishwa kwa

Amiri wa Hizb ut Tahrir

Sheikh Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Katika Ukurasa Wake wa Facebook

Jibu la Swali:

Kuwa ndani na Kujishughulisha na Majeshi ya Tawala Zilizopo katika Nchi za Kiislamu
Kwa: Mubdeen
(Imetafsiriwa)

Swali:

Swali, ikiwa utaruhusu: Ni ipi hukmu ya Kiislamu ya kuwa ndani na kujiunga na majeshi ya tawala hizi? Je, inajuzu kwa kijana kufanya kazi ndani ya majeshi ya tawala za sasa na kupandishwa vyeo ...

Jibu:

Wassalamu alaikum wa Rahmatullah wa Barakatahu,

1- Siku za nyuma tulitoa taarifa mnamo 8/6/2013 kuhusiana na kufanya kazi kama koplo au polisi... na ilieleza:

[- Abu Ya’la imesimulia katika Musnad yake na Ibn Hibban katika Sahih yake, na maneno ni ya Abu Ya’la: Kutoka kwa Abu Sa’id na Abu Hurairah, aliyesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema:

«لَيَأْتِيَنَّ عَلَى النَّاسِ زَمَانٌ يَكُونُ عَلَيْكُمْ أُمَرَاءُ سُفَهَاءُ يُقَدِّمُونَ شِرَارَ النَّاسِ، وَيَظْهَرُونَ بِخِيَارِهِمْ، وَيُؤَخِّرُونَ الصَّلَاةَ عَنْ مَوَاقِيتِهَا، فَمَنْ أَدْرَكَ ذَلِكَ مِنْكُمْ، فَلَا يَكُونَنَّ عَرِيفاً وَلَا شُرْطِيّاً وَلَا جَابِياً وَلَا خَازِناً».

“Utakuja wakati ambapo mtakuwa na watawala wapuuzi na madhalimu juu yenu wanaotanguliza watu waovu zaidi, na kuwafuata katika machaguo yao na wanachelewesha Swala katika nyakati zake zilizowekwa. Kwa hiyo atakayefikiwa na wakati huo miongoni mwenu, basi asiwe koplo, polisi, mtoza ushuru wala mweka hazina...” Katika hadith hii, Mtume (saw) anakataza kabisa hawa wanne chini ya utawala wa watawala wapumbavu.

Lakini Al-Tabarani amesimulia katika Al-Saghir na Al-Awsat kutoka kwa Abu Huraira riwaya ifuatayo:

«فَمَنْ أَدْرَكَ مِنْكُمْ ذَلِكَ الزَّمَانَ فَلَا يَكُونَنَّ لَهُمْ جَابِياً، وَلَا عَرِيفاً، وَلَا شُرْطِيّاً»

“Yeyote atakayefikiwa na wakati huo miongoni mwenu, basi asiwe kwao mtoza ushuru, wala koplo wala polisi.” Kwa hivyo, asema: «فَلَا يَكُونَنَّ لَهُمْ» “Basi asiwe kwao.” Yaani, katazo hilo limewekewa mipaka kwa sababu “اللام” ni kwa ajili ya takhsisi, na hii ina maana kwamba uharamu katika Hadith ya pili unahusiana na kazi za watawala hawa, kama vile walinzi wao binafsi, idara za usalama zilizowekwa kwa ajili ya ulinzi wao, pamoja na mlinzi wa fedha zao, na idara nyingine za usalama zilizopangiwa watawala... Kwa sababu kanuni za msingi zinaeleza kuwa hukmu jumla inatumika kwa iliyofanyiwa takhsisi, basi katazo hilo linahusiana na kufanya kazi katika vyombo vya polisi vilivyobobea katika ulinzi na usalama wa watawala... Kuhusu vyombo vyengine vya polisi vya kawaida, inaruhusiwa. Bila shaka, kuruhusiwa hakumaanishi kuwaonea watu au kuwanyima haki zao, bali ni kutafuta haki katika kazi... Rajab Al-Fard 29, 1434 H - 8 Juni 2013]

*Polisi waliotajwa katika Hadith hii ni kama ilivyoelezwa katika Lisan al-Arab na Ibn Manzur:

[Na mtu akajiweka hivi na hivi, amefanya ijulikane kwake na ajitayarishe, na kutokana nayo sharti hilo likaitwa kwa sababu walijifanyia ishara ambayo kwayo walimtambulisha mtu mmoja kuwa ni polisi.... polisi katika Sultan ni wa ishara na maandalizi, na polisi na mtu anayehusishwa na polisi, na wingi ni sharti. Waliitwa hivyo kwa sababu walijiandaa kwa hilo na wakajijulisha ishara, na ikasemekana wao ndio kikosi cha kwanza kushuhudia vita...]

* Imeelezwa katika Kamusi ya Al-Muhit na Al-Fayrouzabadi: [Na polisi, kwa ḍham (بالضم): mliyoyawekea masharti, husemwa: Lolote mlilo faradhisha, husemwa: Chukueni sharti lenu, na sharti mojawapo ni kama uzi, na wao ndio kikosi cha kwanza kushuhudia vita na kujiandaa kwa ajili ya kifo, na kundi la wasaidizi wa magavana, naye ni polisi kama Waturuki na Jahani, waliitwa hivyo kwa sababu walijitambulisha kwa ishara ambazo watajulikana nazo.]

Kwa hivyo, kinachomhusu polisi kinamhusu askari iwapo inajuzu au la. Kwa hiyo, kufanya kazi katika jeshi katika nchi za Kiislamu inajuzu isipokuwa ikiwa ni kikosi maalum cha kumlinda mtawala asiyetawala kwa mujibu wa Uislamu, kumkusanyia fedha, na kuzilinda fedha hizi. Ikiwa alikuwa katika kikosi maalum cha kumlinda mtawala na pesa zake, basi ni haramu. Lakini ikiwa kazi yake katika jeshi ni kwa ajili ya mengine yasiyokuwa hayo, basi inajuzu. Bila shaka, kuruhusiwa hakumaanishi kuwakandamiza watu au kuwanyima haki zao, bali ni kutafuta haki katika kazi, kuifanya vizuri kwa ukamilifu.

Natumai hii inatosha, na Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi.

Ndugu Yenu,

Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah

17 Sha’ban 1445 H

Sawia na 27/02/2024 M

Link ya jibu hili kutoka ukurasa wa Amiri wa Facebook

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu