Jumapili, 22 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Trump na Netanyahu Wanajigamba na Kujisifu Huku Watawala Wetu Wakikaa Kimya Mithili ya Wafu Makaburini Mwao!

Vita kati ya Iran na umbile la Kiyahudi vimemalizika, na jinai za Mayahudi mjini Gaza hazikukoma wakati wa vita hivyo, wala hadi wakati huu. Marekani ilifanya ujanja wa kiusanii, ikidai kuwa imeangamiza uwezo wa nyuklia wa Iran. Hatua hii imekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kukutana na wale wanaojiita mawaziri wa Troika wa Ulaya, ambao walikuwa sehemu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran kabla ya Marekani kujitoa katika mazungumzo hayo wakati wa muhula wa kwanza wa Trump. Iran pia ilifanya mbwembwe za kiusanii kwa kurusha makombora kadhaa katika Kambi ya Kimarekani ya Al Udeid nchini Qatar, baada ya kuifahamisha Marekani kuhusu hilo, kama Trump mwenyewe alivyosema.

Harakati ya Taliban na Fursa ya Kusimamisha Khilafah

Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.

Uamuzi wa Mahakama ya Upeo Unaipa Zinaa Nafasi sawa na Ndoa

Mahakama ya Upeo imeamua kuwa watoto waliozaliwa nje ya ndoa na baba Waislamu wana haki ya kurithi mali ya baba yao, jambo linaloashiria maendeleo makubwa katika tafsiri ya sheria za kibinafsi za Kiislamu nchini Kenya. Hii ni baada ya Mahakama ya Juu mnamo Jumatatu tarehe 30 Juni kutupilia mbali rufaa ya Fatuma Athman Abud Faraj, ambaye alitaka kuwatenga watoto wa marehemu mumewe, Salim Juma Hakeem Kitendo, katika mali yake kwa madai kwamba walizaliwa nje ya ndoa inayotambulika ya Kiislamu.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu