Jumapili, 27 Safar 1446 | 2024/09/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Ardhi ya Baraka-Palestina

H.  25 Muharram 1446 Na: BN/S 1446 / 03
M.  Jumapili, 21 Julai 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Mkono wa Umbile Halifu Wavamia nchi Yetu ya Yemen na ash-Sham chini ya Njama za Tawala na Kukosekana kwa Uzuiaji
(Imetafsiriwa)

Ndege za umbile halifu la Kiyahudi zilianzisha msururu wa mashambulizi ya kichokozi dhidi ya Yemen. Wakati wa mkutano wake jana, Baraza la Mawaziri la umbile hilo linalohusika na masuala ya usalama liliidhinisha shambulizi hilo dhidi ya Yemen, kwani uvamizi huo ulilenga vituo vya kuhifadhi mafuta na kituo cha umeme katika bandari ya Hodeidah.

Umbile halifu la Kiyahudi halifungi tena jinai zake kwa Palestina na watu wake, ambapo linatekeleza ukandamizaji, uchokozi, ufisadi ardhini, mauaji, na ukiukaji wa matukufu. Bali mkono wake wa dhambi umekuwa mrefu na mrefu katika uchokozi wake kila siku, na sasa unaifikia Yemen ya imani na hekima, na Mayahudi wameanza kumwaga damu za Waislamu wanavyotaka, na kuteketeza ardhi yao watakavyo, halafu wanajisifu, ambapo waziri wa jeshi wa umbile hilo anasema moto uliozuka Yemen “unaonekana kote Mashariki ya Kati na umuhimu wake uko wazi. Tutafanya hivi mahali popote panapohitajika.” Waoga hawa wa kuchukiza hawakuweza kupanua uchokozi wao, kujivunia vitisho vyao, na kujivunia kile wanachokielezea kama “kuzuiwa” lau si kwa uwepo wa watawala vibaraka ambao uoga wao ulizidi uoga wowote, na ambao walipitiliza mipaka yote katika kimya chao, usaliti, na njama.

Watawala wa Waislamu hawakuuachia Umma mpaka uliolindwa, wala upande wa kuogopwa, wala mstari mwekundu ambao ungehifadhi maisha na heshima yake. Uchokozi wa leo, hata kama ulikuwa mpya dhidi ya Yemen wa umbile oga, ulitanguliwa na umwagaji damu huko Palestina na kukiuka utukufu wa Msikiti wa Al-Aqsa, na ulitanguliwa na uchokozi dhidi ya Lebanon, na kwa kukiuka Syria, ambayo ina “haki ya kujibu” bila ya jibu! Ndege za umbile hilo pia zimewahi kuruka katika anga za Sinai, Tunisia na Sudan, na kwa nchi zilizosalia ambazo bado hazijaguswa na moto wa umbile hilo au mkono wa ufisadi wake, zinasubiri zamu yao ifuate katika uchokozi wake. Utiifu, udhalilifu, na njama za watawala wake havitachelewesha kuathiriwa na ufisadi na uovu wa umbile hilo.

Enyi Waislamu, na enyi Wana wa Waislamu, Askari, Maafisa na Majeshi!

Nyinyi ni Umma wenye Aqida (itikadi) na ushujaa, watu wa vifaa na idadi, na izza yenu kwa Mwenyezi Mungu na Dini yenu ni Aqida. Kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, je, munakubali kwamba ndugu wa nyani na nguruwe wanakunyanyaseni katika al-Sham yenu na kukupigeni katika Yemen yenu?! Mnawezaje kukaa kimya juu ya watawala waliokaa kimya juu ya kumwagwa damu yenu, kudhuru utu wenu, na kumuunga mkono adui yenu dhidi yenu?!

Kukosekana kwa kizuizi kinachozuia umbile hili nyakuzi, kukata mkono wa uchokozi wake, kung'oa mizizi yake, na kumaliza uovu wake, kumelifanya liendelee katika udhalimu wake, na kuonyesha mateso yake kwa wote wanaoonyesha upinzani. Watawala wenu wa ngurumo sio ngao kwenu, wala sio kizuizi kwa adui yenu. Wanajibu tu uhalifu wao kwa utiifu na udhalilifu na utiifu zaidi. Bali wao ni walaghai nyuma ya pazia. Kwa hiyo, imekuwa ni lazima kuwaondoa na kuachana nao, au hata ni umuhimu kabisa, na kuweka uongozi wa kijasiri na uaminifu. Khalifa anayesimamisha Dini ya Mwenyezi Mungu, anayepigana jihad kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na asiyemuogopa yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu. Tunaomba tuokolewe kutokana na umbile hili la kihalifu, hasa kwa vile madhara, uovu na uchokozi wake umevuka Palestina na watu wake na sasa unaathiri kila mtu karibu nayo.

[وَلَيَنصُرَنَّ اللهُ مَن يَنصُرُهُ إِنَّ اللهَ لَقَوِيٌّ عَزِيز]

“Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anaye msaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu.” [Al-Hajj 22:40]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa – Palestina

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Ardhi ya Baraka-Palestina
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu