Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Mpeni Raj Mkoloni Amerika Inayoporomoka Msukumo wa Mwisho kwa Kuziunganisha Pakistan, Afghanistan na Asia ya Kati kama Dola Moja ya Kiislamu ya Khilafah

(Imetafsiriwa)

Leo, 7 Muharram 1443 H, 15 Agosti 2021, Waislamu walilipuka kwa furaha wakati mujahidina wa Afghanistan waliingia Kabul, huku Amerika ikiondoka kwa haraka na kibaraka wa Magharibi Ashraf Ghani akikimbia. Kwa hivyo, mujahidina elfu chache, wenye silaha duni, wakikikanyaga kanyaga kiburi cha dola ya tatu ya wakoloni chini ya miguu yao, kama vile watangulizi wao walivyofanya dhidi ya Urusi ya Usovieti na Dola ya Uingereza hapo awali. Kuna kasi sasa ya kuhakikisha miundombinu ya kikanda ya Amerika imeng'olewa kabisa, kama kiasi ya kwamba kamwe haitaweza kukua tena, kama vile uvamizi wa Raj wa Kiingereza na Urusi ya Usovieti haukuwahi kufanya, baada ya kuondolewa kwa vikosi.

Enyi Waislamu wa Pakistan!

Ni wakati sasa wa kumpa Raj mkoloni wa Kiamerika msukumo wa mwisho.

Kuna kasi sasa ya kutaka kukataliwa kwa laini za usambazaji za ALOC na GLOC ambazo hupita kwenye anga zetu na ardhi yetu, kwani ndizo laini muhimu za uhai wa miundombinu ya kieneo ya Amerika. Maadamu watawala wa Pakistan watazibakisha wazi laini za usambazaji za Amerika, uwepo haribifu wa Amerika utabakia na kukua tena.

Kuna kasi sasa ya kutaka kufungwa kwa vituo vya ujasusi katika ubalozi wa Amerika jijini Islamabad na ubalozi wa Amerika jijini Karachi. Wao ni macho ya uingiliaji ambayo yamekodoka masaa ishirini na nne kwa siku, siku saba kwa wiki, ambayo bila kwayo miundombinu yote ya Amerika itakuwa kipofu. Maadamu watawala wa Pakistan wanaruhusu vituo hivyo vya ujasusi vya Amerika kuwepo, mawasiliano yetu nyeti ya kijeshi na kijasusi yote yameathiriwa, na kuiwezesha Amerika kubaki katika kanda yetu.

Kuna kasi sasa ya kutaka kumalizwa kwa uwezeshaji mazungumzo kati ya Amerika, mawakala wake na mujahidina wa Afghanistan. Ni mtindo hadaifu wa makafiri wa kuwapa ofa Waislamu ya mazungumzo ili kuwasababishia hasara na kuvua idhini kutoka kwao, wakati wanajua kwamba Umma wa Kiislamu unaweza kuchukua haki yake kamili kwenye uwanja wa vita, bila makubaliano yoyote au hasara. Maadamu watawala wa Pakistan wanaendelea kuwezesha mazungumzo hayo, hii ni njia ya adui kuingia kwenye ngome kupitia mlango wa nyuma, baada ya kuondoka kupitia mlango wa mbele.

Ni wakati sasa kumpa Raj mkoloni anayeporomoka Amerika msukumo wa mwisho, kwa kutaka kukomeshwa kwa miungano yote ya kijeshi na mafungamano ya kiuchumi na Amerika, kwani ni adui wa wazi wa Waislamu na Uislamu, huku akiwaunga mkono wengine katika uadui wao. Lazima tujitenge mbali na dhambi hili kubwa la watawala hawa, ili tuwe mbali na Hasira na Adhabu ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) asema,

]إِنَّمَا يَنْهَاكُمْ اللَّهُ عَنْ الَّذِينَ قَاتَلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَأَخْرَجُوكُمْ مِنْ دِيَارِكُمْ وَظَاهَرُوا عَلَى إِخْرَاجِكُمْ أَنْ تَوَلَّوْهُمْ وَمَنْ يَتَوَلَّهُمْ فَأُوْلَئِكَ هُمْ الظَّالِمُونَ]

“Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kufanya urafiki na wale walio kupigeni vita, na wakakutoeni makwenu, na wakasaidia katika kufukuzwa kwenu. Na wanao wafanya hao marafiki basi hao ndio madhaalimu.” [Surah al-Mumtahina 60:9].

Enyi Waislamu wa Jeshi la Pakistan na Mujahidina!

Ziunganisheni Pakistan, Afghanistan na Asia ya Kati kama Dola Moja ya Khilafah

Jueni kwamba mipaka kati ya nchi za Waislamu ni mtindo wa wakoloni wa kutudhoofisha, kutugawanya na kututawala, wakati nguvu zetu ziko katika kuungana kwetu kama dola moja, chini ya bendera ya Uislamu. Katika kanda yetu, ni Msitari wa Durand ndio uliyoiacha Afghanistan kuwa ndogo na dhaifu, ikikabiliwa na kuingiliwa mara kwa mara, mpenyo na uvamizi wa maadui wa Umma wa Kiislamu, iwe ni Urusi kabla ya 1989 au India na Amerika tangu 2001. Ni Msitari wa Durand ndio ulioawafanya Waislamu watukufu wa Afghanistan kuwa waathiriwa na wakimbizi katika kanda yetu, kupitia michezo mikubwa, njama na unafiki, na kusababisha kuuawa kwao kwa mamia ya maelfu. Ni Msitari wa Durand ndio uliojenga mashaka, chuki na uhasama kati ya Waislamu, ukigawanya safu zao, ili makafiri waweze kuingia kati yao kama mashetani wavurugaji, kuanzia Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi.

Njia sahihi ya kuzuia maadui kuingia katika mageti ya kanda yetu tangu mwanzo, ni kuyaimarisha, kwa kuziunganisha Pakistan, Afghanistan na Asia ya Kati kama dola moja ya Kiislamu ya Khilafah. Kwa kweli, nguvu zetu haziko katika kutegemea, muungano na utegemezi wa maadui wa Waislamu, iwe ni China upande wa Mashariki au Amerika upande wa Magharibi. Kuimarika kwetu kunategemea tu kuungana kwa Ummah wa Muhammad (saw) kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (swt), kama ndugu moja na kama dola moja, na jeshi moja na uchumi mmoja, chini ya Khaleefah mmoja, akitawala kwa yale yote aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) asema,

]الَّذِينَ يَتَّخِذُونَ الْكَافِرِينَ أَوْلِيَاءَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ أَيَبْتَغُونَ عِندَهُمُ الْعِزَّةَ فَإِنَّ الْعِزَّةَ لِلَّهِ جَمِيعًا]

“Wale ambao huwafanya makafiri kuwa ndio marafiki badala ya Waumini. Je! Wanataka wapate kwao utukufu? Basi hakika utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu.” [Surah An-Nisa’a 4:139]. Ni juu yenu sasa kuunganisha nguvu zenu kwa kuubomoa Mstari wa Durand, ambao unakugawanyeni na kukudhoofisheni mbele ya maadui zenu, mkisimama katika safu moja kama ndugu dhidi ya Waamerika na Wahindi sasa, kama mlivyofanya dhidi ya Warusi wa Usovieti hapo awali.

Upuuzeni mfumo wa kimataifa au idhini ya walezi wake wa kikoloni, kwani kama mazungumzo, ni mtego wa kuunyima Umma wa Kiislamu kile mnachoweza kukikamata kwa ajili yake kwa jasho lenu, damu zenu, moto wenu na chuma chenu katika Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt). Mfumo wa kimataifa ni mfumo wa dola za kihalifu za zama zetu, ambazo zimenyonya sehemu kubwa ya ulimwengu bila ya chembe ya huruma, kuanzia Latin Amerika hadi Kusini Mashariki mwa Asia. Ni mfumo ulioundwa na watangulizi waovu wa watawala wa sasa wa Kimagharibi, kudhibiti maendeleo yasiyokoma ya dola ya Khilafah, wakati majeshi yake yalipofikia magetini mwa miji mikuu ya Magharibi. Ni mfumo huu wa makruseda wa kidhalimu ndio ulionyima ukombozi wa Ardhi Iliyobarikiwa - Palestina, Kashmir Iliyokaliwa na Ardhi zengine za Kiislamu zilizokaliwa kwa muda mrefu, licha ya uwepo wa mamilioni ya wanajeshi wa Kiislamu walio tayari na wenye uwezo. Leo, baraka iwe kwa Dini ya Haki, Umma wa Kiislamu una rasilimali nyingi na nguvu kazi ya kubomoa mfumo huu fisidifu, ukitoa wanadamu afueni inayohitajika mno, huku ukianzisha mfumo safi uliojengwa juu ya maamrisho ya Mwenyezi Mungu (swt), kama ulivyofanya kwa karne nyingi nyuma, katika zama za Khilafah.

Inatosha sasa kwa udanganyifu, uwongo, mitego na usaliti wa watawala wa sasa wa Waislamu. Wao ni mzigo ambao lazima sasa uondolewe kutoka kwa Ummah kupitia mikono yenu. Toeni Nussrah yenu sasa kwa Hizb ut Tahrir ili kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume, itakayokusanya nguvu za kijeshi za Umma na rasilimali za kiuchumi, kumrarua Raj mkoloni Amerika inayoanguka na kuasisi utawala wa kikanda wa Khilafah, njiani kuelekea kuwa dola inayoongoza duniani. Mwenyezi Mungu (swt) asema,

إِن يَنصُرۡكُمُ ٱللَّهُ فَلَا غَالِبَ لَكُمۡ وَإِن يَخۡذُلۡكُمۡ فَمَن ذَا ٱلَّذِي يَنصُرُكُم مِّن بَعۡدِهِ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ]

“Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wa kukushindeni, na akikutupeni ni nani, basi, baada yake Yeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.”             [ Surah Aali-Imran 3:160].

H. 7 Muharram 1443
M. : Jumapili, 15 Agosti 2021

Hizb-ut-Tahrir
Wilayah Pakistan

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu