Alhamisi, 15 Muharram 1447 | 2025/07/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi

Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."

Soma zaidi...

Kutoka Pakistan hadi ash-Sham: Je, Kweli Tulimshinda Bashar au Tulimbadilisha tu kwa Nakala zake?!

Wakati miji yote ilipokombolewa kutoka mikononi mwa dhalimu wa ash-Sham, Bashar, tulifikiri ushindi ulikuwa umefika. Tuliamini kuwa wakati umefika wa kusimamishwa Khilafah kwa njia ya Utume—hali ile ile iliyobashiriwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)—ambayo itatawala kwa Qur’an na Sunnah na ilionekana iko tu kwenye kona. Walakini, kuvunjwa moyo kulilingana na ukubwa wa mihanga, na usaliti ulifuata takriban miezi sita baada ya wanamapinduzi kuingia Damascus kwa takbira na shangwe za ushindi. Usaliti ulikuja kutoka kwa wale tuliotarajia wangejenga upya juu ya magofu—sio kujisalimisha kwao!

Soma zaidi...

Mstari Mwekundu wa Unafiki: Jinsi Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Yanavyofichua Nyuso

Mnamo Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, kitovu cha kisiasa cha Uholanzi kiligeuka kuwa chekundu. Maelfu ya watu walijiunga na maandamano jijini The Hague, ambapo mstari mwekundu wa ishara ulichorwa - mstari unaoashiria mpaka wa maadili wa kile ambacho bado kingali kinaweza kutetewa. Kichocheo hakikuwa tu ushiriki wa ‘Israel’ katika Shindano la Nyimbo la Eurovision, bali zaidi ya yote ni kuongezeka kwa hasira juu ya baa la njaa mjini Gaza na kutochukua hatua kwa aibu kwa serikali za Magharibi.

Soma zaidi...

Harakati ya Taliban na Fursa ya Kusimamisha Khilafah

Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli Mpaka Siku ya Mwisho ni kwa Umma wa Kiislamu Pekee

Hata leo, katikati ya misiba isiyohesabika na isiyoweza kuvumilika, Ummah huu umethibitika kuwa thabiti katika kitambulisho chake na hivyo hauwezi kuangamizwa. Imethibitika kuwa unastahiki vyeo ulivyotunukiwa na Mola wa walimwengu, Mwenyezi Mungu Azza wa Jall! Angalia Kashmir, India, Afghanistan... Angalia Waislamu wa Syria, Turkestan Mashariki, Myanmar, katika nchi za Afrika, duniani kote, na mwisho kabisa Waislamu wa Palestina na hasa Gaza! Magaidi hao wa Kizayuni wameshindwa katika kila lengo lao kuhusu Gaza. Ummah huu umethibitisha mara kwa mara, kwamba uwepo wake hauzimiki! Hata adui zake wawe wakatili kiasi gani!

Soma zaidi...

Je, Mafanikio kwa Waislamu yanaweza Kupatikana kupitia Siasa za Kidemokrasia?

Kutokana na mauaji makubwa ya halaiki yanayotokea Gaza na dori ya Marekani katika kusaidia na kuunga mkono yaendelee, kumekuwa na mijadala mingi miongoni mwa Waislamu kuhusu jinsi ya kujihusisha zaidi kisiasa na jinsi jamii ya Kiislamu inavyoweza kuwa mstari wa mbele katika kuunda siasa za Marekani ili kubadilisha dunia kuwa bora. Ndani ya mijadala hii, mengi yanasemwa kuhusu kujishughulisha na uraia, kujiunga na kuunga mkono wagombea mahususi wa kisiasa, kunyima kura zao kama aina ya adhabu, na hatimaye kupata Waislamu zaidi, au "washirika" kwenye nyadhifa katika ngazi za dola na majimbo. Kuna gumzo hata miongoni mwa kina dada wakidai kwa furaha kwamba wanajaribu kumlea kijana au binti yao kuwa Rais wa kwanza wa Marekani Muislamu. Haya yanawekwa kama mafanikio sio tu kwa Waislamu wa Amerika, lakini Waislamu kote ulimwenguni. Huu unawekwa kama mpango wa mafanikio licha ya ukweli kwamba vyama vyote vya kisiasa, iwe vya rangi ya samawati, nyekundu, au kijani vinaunga mkono umbile la Kizayuni, au dola zengine zenye kufanya mauaji ya halaiki mithili ya China na India.

Soma zaidi...

Wanawake Waliofaulu katika Uislamu wana Sifa hizi

Katika Uislamu, hakuna fahamu ya kuingia Jannat kulingana na nani unamjua na hadhi yako ya kidunia ni ipi. Wote walisifiwa na Mwenyezi Mungu (swt) kwa sababu ya sifa zao za pamoja za kuwa karibu katika utendaji wao wa kuwa kama mfano wa Mtume (saw). Ikiwa tunataka hadhi sawa ya kuingia Jannat lazima basi tufuate mfano wao wa kufanikiwa. Sifa zifuatazo basi zinahitajika.

Soma zaidi...

Vipi Tunaweza Kuwa Miongoni Mwa Wenye Mafanikio hapa Duniani na Akhera?

Mafanikio yanazunguka ulimwengu huu na Akhera, anayemcha Mwenyezi Mungu (swt) humsahilishia mambo yake, hubariki matendo yake, huitengenezea nafsi yake, mke wake na watoto wake, humpa njia ya kutokea katika matatizo, humruzuku kutoka katika vyanzo asivyotarajia, na humtosheleza. Zaidi ya hayo, Yeye (swt) humlipa sana subira yake wakati wa matatizo. Wengine wamesema: "Mafanikio ni kupata ushindi na kufikia lengo la mtu. Katika dunia hii, maana yake ni kupata furaha inayoleta kutosheka katika maisha. Katika Akhera, ina jumuisha mambo manne: uwepo milele usio na mwisho, heshima bila fedheha, mali bila umasikini, na elimu bila ya ujinga."

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli: Safari Inayoanza Ramadhan

Ramadhan inapoingia katika maisha yetu kila mwaka, huleta mabadiliko-wakati wa uwazi ambapo tunarudi nyuma kutoka kwa mazoea yetu ya kila siku na kujiuliza maswali ya kina. Ni mwezi ambapo kwa kawaida tunatathmini upya uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu (swt), vipaumbele vyetu, na mwelekeo wa maisha yetu. Katika wakati huu mtakatifu, tunaanza kutafakari: Je, Mafanikio yanamaanisha nini hasa?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu