Kuna Kamba ya Uokozi kwa Sudan – Ichukueni!
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa zaidi ya miaka mia moja, ulimwengu umefanywa kuamini kuwa vita katika Ardhi za Waislamu, hususan nchi za Kiafrika, vinatokana na wao kutoendelea kifikra, kisiasa na kiuchumi. Zimewasilishwa kwa ulimwengu kuwa haziwezi kusimamia uwepo wao bila kile kinachoitwa msaada na uingiliaji kutoka kwa Magharibi.