Alhamisi, 10 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mpango wa Trump ni Sumu Hatari, Ukaliaji Kimabavu wa Marekani na Umoja wa Mataifa wa Gaza, na Uhalifu Mkubwa Uliofanywa na Watawala wa Waislamu

Kujisalimisha na kutoa silaha, kuregeshwa kwa mateka na mabaki ya wafu, na uvamizi unaoongozwa na Marekani, inayoongozwa na Trump kwa jina la Baraza la Amani, likisaidiwa na mwenye chuki dhidi ya Uislamu, Tony Blair, na kutekelezwa na tawala za eneo hili – hizi ndizo sifa za mpango mpya wa Trump, ambao aliutangaza. Amewashukuru viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu na washirika wake barani Ulaya kwa mwitikio wao wa dhati kwake, na kutangaza kuwa viongozi wa eneo hilo wanashiriki kikamilifu katika mpango huo wa amani.

Soma zaidi...

Enyi Wanajeshi wa Misri (Kinana): Vivuko vya Gaza havihitaji Malori, Bali vinahitaji Majeshi na Magari ya Kivita

Hali ya kibinadamu mjini Gaza imefikia viwango vya maafa ambavyo havijawahi kushuhudiwa. Idadi ya vifo vya mashahidi imezidi 65,000. Ripoti za kimataifa zinaweka idadi hiyo kuwa 40% zaidi. Hao ni zaidi ya mashahidi 100,000 na takriban wakimbizi wa ndani milioni 1.9, ambao ni karibu asilimia 90 ya wakaazi wa Ukanda wa Gaza, ambao wanaishi katika mazingira yasiyo ya kibinadamu, na kunyimwa mahitaji ya kimsingi ya maisha. Gaza inakabiliwa na njaa ya kweli, haswa katika sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo. Hospitali zinafanya kazi chini ya 30% ya uwezo wao, na uhaba wa dawa na mafuta unaweka makumi ya maelfu ya wagonjwa katika hatari ya kifo cha polepole. Takwimu hizi zinafichua ukubwa wa maafa hayo na kuthibitisha kuwa kinachoendelea ni vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Gaza.

Soma zaidi...

Msimamo kwa Sherehe za Maadhimisho ya Mapinduzi Mawili ya Septemba Moja yaliingiza Usekula nchini Yemen na Mengine Yalitoa Wito wa Kuuimarisha!

Katika mwezi wa Septemba wa kila mwaka Yemen ina matukio mawili; la kwanza mnamo tarehe 26 Septemba 1962 ambayo ni kumbukumbu ya kupinduliwa kwa mfumo wa kifalme nchini Yemen Kaskazini, na la pili mnamo tarehe 21 Septemba 2014 ambayo ni kumbukumbu ya kuingia kwa Mahouthi jijini Sana’a ambayo ilisababisha udhibiti wao wa mikoa ya kaskazini.

Soma zaidi...

“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”

Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.

Soma zaidi...

Maradhi ya Mkurupuko Yawaangamiza Watu kwa Kukosekana kwa Dola ya Ustawi

Maradhi matatu ya kimazingira—kipindupindu, homa ya dengue, na malaria—yanawaangamiza watu katika majimbo ya Khartoum, Al-Jazirah, na Darfur, katikati ya uzembe wa kutisha na aibu ya kukosekana kwa serikali inayojiita “Serikali ya Matumaini”! Kuna matumaini aina gani wakati watu wanaishi katika mazingira yasiyostahili hata kwa wanyama—mazingira yanayotawaliwa na waenezaji magonjwa, ikiwemo mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Ya‘qub Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, atakuwa mgeni, chini ya kichwa: Ulaya na Ushawishi Wake kwa Matukio nchini Sudan.

Soma zaidi...

Kujibu Matamshi ya Mjumbe wa Marekani Tom Barrack

Kwa mara nyingine tena utawala wa Marekani unaonyesha sura yake halisi kupitia taarifa za mjumbe wake Tom Barrack, katika mahojiano yake yaliyotangazwa na Sky News na mtangazaji mkuu wa IMI International Hadley Gamble, ambaye alijiruhusu kuingilia waziwazi katika masuala ya Lebanon na kubainisha sifa za dori za taasisi ya Jeshi.

Soma zaidi...

Kutoka Uingereza hadi Australia: Utambuzi wa Uongo Unafungua Njia ya Uhalalishaji Mpana zaidi wa Mahusiano

Miaka miwili baada ya mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kizayuni katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, likiungwa mkono kikamilifu na Marekani, NATO, na washirika wao makruseda, Umoja wa Mataifa na dola zenye nguvu duniani wamejibu kwa kulituza umbile hilo. Utambuzi wa “Dola ya Palestina” unakuja huku Gaza ikivuja damu, na baada ya dola 150+ tayari kutoa utambuzi sawia.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu