Ijumaa, 18 Sha'aban 1447 | 2026/02/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Matukio nchini Syria na Kurudi Nyuma kwa Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria

Matukio yanatokea kwa kasi kubwa kaskazini mashariki mwa Syria, na Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria (SDF) vinapoteza udhibiti wa maeneo hayo kwa kasi kubwa, huku serikali ya Syria ikiyachukua. Yote haya yalitokeaje? Hili linapaswa kuelewekaje ikizingatiwa kwamba serikali na SDF ni vibaraka wa Amerika? Na licha ya idhini ya Marekani kwa serikali ya Syria kuwa wazi kama mwanga wa mchana katika kuteka maeneo hayo, utawala wa Trump unapanga nini nchini Syria au viunga vyake?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ni Yapi Yaliyo Nyuma ya Ongezeko la Mgogoro wa Yemen

Baada ya vikosi vya Baraza la Mpito la Kusini (STC) nchini Yemen, vikiongozwa na Aidarus al-Zubaidi, mjumbe wa Baraza la Rais, kupeleka vikosi vyao huko Hadramawt na al-Mahrah, hali ikawa ngumu sana. Rais wa STC Rashad al-Alimi alisitisha makubaliano ya pamoja ya ulinzi na Imarati na kudai kwamba iondoe vikosi vyake kutoka Yemen ndani ya masaa 24. Saudi Arabia ilimuunga mkono mara moja na kushambulia silaha za Imarati katika Bandari ya Mukalla. Kisha Saudi Arabia ilidai kwamba Imarati itii matakwa ya Rashad al-Alimi na kuondoa vikosi vyake kutoka Yemen. Imarati baadaye iliondoka, na hatimaye, al-Zubaidi alikimbilia Imarati. Kwa hivyo, ni nini kilicho nyuma ya kuongezeka huku kwa mgogoro wa Yemen? Je, Uingereza inapoteza washirika wake nchini Yemen? Na je, mzozo huu una vipimo vya kimataifa?

Soma zaidi...

Hotuba ya Mwanachuoni na Amiri wa Hizb ut Tahrir Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah (Mwenyezi Mungu amlinde) Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika siku hizi kama hizi, miaka 105 iliyopita, mwishoni mwa Rajab 1342 H, sambamba na mapema Machi 1924 M, wakoloni makafiri, wakiongozwa na Uingereza wakati huo, kwa ushirikiano na wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, waliweza kuivunja Khilafah. Mhalifu wa zama hizo, Mustafa Kemal, alitangaza ukafiri wa wazi kwa kuifuta Khilafah, kumzingira Khalifa jijini Istanbul, na kumfukuza alfajiri siku hiyo hiyo. Hivyo, tetemeko baya la ardhi lilizikumba ardhi za Waislamu kwa kuvunjwa Khilafah, chimbuko la izza yao na radhi ya Mola wao Mlezi.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: China na Ukombozi Wake Kutoka kwa Mtazamo Wake Mdogo wa Kikanda

 “China inamiliki hisia ya nguvu na mapambano, na kama lengo la China halikufungika tu na kudumisha eneo lake, na kukubali kukabiliana na Amerika kama jibu tu kwa harakati za Amerika kuelekea eneo lake, China haisubutu kupambana na Amerika katika maeneo yao ya ushawishi... na kama isingeanza kutumia ubepari katika nyanja nyingi, haswa katika uchumi... ingekuwa na sauti kubwa kimataifa, na athari yake kwa maslahi ya Amerika ingekuwa na nguvu zaidi. China kwa vyovyote vile ina hisia kali ya nguvu, na inafanya kazi ili kudumisha ubwana wa eneo lake, hata kama iko katika eneo lake...” — Kwa hivyo, je, kizuizi cha China cha mauzo ya nje ya madini adimu ya ardhini kwenda Amerika, kuyauza kwa dhamana za Hazina ya Marekani, kulisasisha jeshi lake, na kujenga jengo kubwa zaidi la kijeshi duniani kusini magharibi mwa Beijing... je, hiki si kiashiria cha ukombozi wa China kutoka kwa mtazamo wake wa kisiasa uliofungika katika eneo lake na upanuzi wa mtazamo huu kushindana na Amerika duniani kote?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ruwaza ya Marekani ya Kutatua Kadhia ya Cyprus

“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Sudan Baada ya Vikosi vya Msaada wa Haraka Kuchukua Udhibiti wa El Fasher

“Massad Boulos, mshauri mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu masuala ya Mashariki ya Kati, alithibitisha kwamba jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka wamekubaliana kusitisha mapigano kwa miezi mitatu, kulingana na mpango wa Quartet, unaojumuisha Imarati, Marekani, Saudi Arabia, na Misri, uliotangazwa mnamo Septemba 12.” (Sky News Arabia, 3/11/2025).

Soma zaidi...

Tanzia ya Mwanachama wa Afisi ya Amiri, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama)

Amiri wa Hizb ut Tahrir, Wanachama wa Afisi ya Amiri, Diwani ya Al-Madhalim (Malalamiko), na Afisi Kuu ya Habari na Hizb ut Tahrir kwa jumla wanaomboleza kwa Umma wa Kiislamu Mwanachama wa Afisi ya AmIrI, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama) aliyefariki dunia asubuhi ya leo, 22 Rabi’ Al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 14 Septemba 2025 M, akiwa na umri wa miaka themanini na saba.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mkakati wa Amerika na Suluhisho la Dola Mbili

Tunajua kwamba mkakati wa Marekani wa kuasisi umbile la Kiyahudi katika moyo wa nchi za Kiislamu, kwa sehemu kubwa, umeegemezwa kwenye suluhisho la dola mbili. Hata hivyo, chini ya Trump, mkakati huu umeanza kuatelekezwa, au angalau kunyamaziwa, jambo ambalo limezua maswali. Kwa mfano, Trump alisema, "Unapotazama ramani, ramani ya Mashariki ya Kati, 'Israel' ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ardhi hizi kubwa mno. Kwa hakika nilisema: 'Je, kuna njia yoyote ya kupata zaidi? Ni ndogo..." (Sky News, 19/8/2024). Je, hii inamaanisha kuwa mradi wa suluhisho la dola mbili wa Amerika umekufa na kukamilika, au bado ungali hai?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu