Kilio kwa Wabebaji Dawah “Mulikuwa wapi Muda wote huu?!”
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika ghururi ya maisha na kutojali kwa jamii, neno moja pekee linabaki kuwa na uwezo wa kutikisa milima, kuchochea dhamiri, na kuamsha ari ya uwajibikaji katika nyoyo za Umma wa Uislamu. Ni neno lililotoka katika vinywa vya wale ambao miili yao ilichakaa kwa mateso na ambao fremu zao zilisagwa kwa dhulma ndani ya magereza ya madhalimu: “Mulikuwa wapi muda wote huu?!” Ilisemwa na mmoja wa wale walioachiliwa huru kutoka magereza ya mtoro Bashar al-Assad, wale walioonja majanga na ambao miaka yao ilizimwa gerezani; alipokutana na baadhi ya watu waliokuwa wameachiliwa huru, hakuuliza kuhusu idadi ya miaka gerezani, badala yake alipiga kelele usoni mwake: “Mulikuwa wapi, mulikuwa wapi muda wote huu? Kwa nini hamkutuachilia huru wakati tulipokuwa tunazikwa tukiwa hai?”