Ijumaa, 11 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kilio kwa Wabebaji Dawah “Mulikuwa wapi Muda wote huu?!”

Katika ghururi ya maisha na kutojali kwa jamii, neno moja pekee linabaki kuwa na uwezo wa kutikisa milima, kuchochea dhamiri, na kuamsha ari ya uwajibikaji katika nyoyo za Umma wa Uislamu. Ni neno lililotoka katika vinywa vya wale ambao miili yao ilichakaa kwa mateso na ambao fremu zao zilisagwa kwa dhulma ndani ya magereza ya madhalimu: “Mulikuwa wapi muda wote huu?!” Ilisemwa na mmoja wa wale walioachiliwa huru kutoka magereza ya mtoro Bashar al-Assad, wale walioonja majanga na ambao miaka yao ilizimwa gerezani; alipokutana na baadhi ya watu waliokuwa wameachiliwa huru, hakuuliza kuhusu idadi ya miaka gerezani, badala yake alipiga kelele usoni mwake: “Mulikuwa wapi, mulikuwa wapi muda wote huu? Kwa nini hamkutuachilia huru wakati tulipokuwa tunazikwa tukiwa hai?”

Soma zaidi...

Sudan: Mfano Mwengine wa Utaifa Uliofeli

Tangu 1945 kumekuwa na angalau nchi mpya 34 ambazo zimetambuliwa na Umoja wa Mataifa. Hili lilitokana na wimbi la utaifa ambalo lilienea kote ulimwenguni kwa miongo kadhaa tangu katikati ya miaka ya 1900. Mipaka ya kindoto ilichorwa ili kutoa uhuru kwa makundi mbalimbali na haki ya kutawala, kwani nchi kama vile Sudan iliyoungana hapo awali zilitumbukia ndani ya mizozo na machafuko.

Soma zaidi...

Khilafah kwa Njia ya Utume: Uadilifu na Rehma kwa Walimwengu

Uislamu ni dini ya haki ya Mwenyezi Mungu, ujumbe wa mwisho wa wahyi wa Mwenyezi Mungu na haki pekee ya kweli. Sheria na itikadi zengine zote duniani leo ni ya batili na potofu. Dini hii imekamilika katika sheria zake, inadhamini uadilifu kamilifu, rehma kamilifu, uongofu kamili, heshima kamilifu, na utumwa kamili kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu inatoka kwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Soma zaidi...

Kwa Uislamu, Watu wa Sudan Wanayeyushwa ndani ya Chungu Kimoja, na Wanaishi Maisha yenye Staha na Haki Chini ya Dola Yake

Idadi ya watu wa Sudan inakadiriwa kufikia milioni 49.4, kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) mwaka 2024. Asilimia tisini na sita ya wakaazi wote ni Waislamu, huku jamii ndogo ya Wakristo na watu binafsi wakifuata dini za kipagani. Jamii ya Wasudan inaundwa na makabila ya asili ya Waarabu, Waafrika, na Wanubi, yakiwakilisha zaidi ya makabila 500. Waarabu wanaunda kabila kuu, linalojumuisha 70% ya idadi ya watu, pamoja na makabila mengine, yakiwemo Beja, Nuba, Fulani, Geberti, Fur, Masalit, na mengineyo.

Soma zaidi...

Khilafah pekee ndio inayojali Maslahi ya Watu na ndio Mlinzi wa Haki na Mahitaji yao

Hali mbaya ambayo Sudan imefikia kufuatia vita vya kikatili vilivyoanza miaka miwili iliyopita kati ya vikosi vya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka sio siri. La kusikitisha, watu wasio na hatia wa Sudan wamelipia, na wanaendelea kulipia, gharama ya mzozo huu mbaya wa kimataifa unaoendeshwa na silaha za ndani kwa lengo la kuichana nchi na kulinda maslahi ya Amerika, Ulaya, na wengineo!!

Soma zaidi...

Hakuna Wokovu kwa Watu wetu nchini Sudan Wala Amani au Usalama isipokuwa chini ya Mfumo wa Uislamu

Katika yote historia, wingi wa makabila nchini Sudan kamwe haukuwa sababu ya mizozo na vita. Bali, kilichosababisha haya ni mapambano makali ya kisiasa na kijeshi baina ya dola za kikoloni na vibaraka wao, ambayo yaliharibu mazao na vizazi, hasa baada ya wao kuigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kimapendeleo, sawa kabisa na yale yanayotokea leo na kwa usahihi kabisa kama ilivyotokea katika siku za mwanzo za Ujahiliya.

Soma zaidi...

Sudan: Giza la Muundo wa Makubaliano au Nuru ya Katiba Inayotokana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ya Mtume Wake?

Haishangazi kwa mtu yeyote anayefuatilia hali ya kisiasa nchini Sudan kujua kwamba vita hivi viliratibiwa na kusimamiwa na Marekani chafu na yenye nia mbaya ili kufanikisha ajenda yake na kuvunja nguvu za washindani wake wa Ulaya, hasa raia wanaoshirikiana na Uingereza. Vita hivi vinafadhiliwa na Amerika, ni mchezo wao uliolaaniwa. Ushahidi wa wazi zaidi ni kwamba taarifa kuhusu kurefusha vita ilitoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Blinken. Kurefushwa kwa vita hivi si kwa ajili ya utatuzi au kuhifadhi damu au kukomesha uharibifu ambao umeharibu nchi na watu wake; badala yake, ni mapambano ya nyuma na mbele na jaribio la kuweka maono ya kisiasa ambayo yanahakikisha na kuhifadhi maslahi ya Marekani nchini.

Soma zaidi...

“Kujitawala Wenyewe” kwa Mujibu wa Matakwa ya Wakoloni!

Ardhi zetu za Kiislamu zimekuwa jukwaa la kupigania mali na ushawishi kati ya Marekani na Ulaya. Cha kusikitisha ni kwamba, zana za mapambano haya ni baadhi ya wana wa Ummah, iwe katika serikali au vuguvugu la waasi, kama inavyotokea leo nchini Sudan, wakati wanaoshindwa pekee katika vita hivi ni watu wasio na hatia, wasio na nguvu.

Soma zaidi...

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu