Jumanne, 24 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa kutenganisha Darfur, Hizb ilifanya Visimamo katika miji kadhaa ya Sudan

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa Marekani wa kuichana nchi hii kwa kuitenganisha Darfur na Sudan, hizb ilifanya kisimamo katika Msikiti wa Al-Aqit mjini Gadharef mnamo siku ya Alhamisi, Septemba 11, 2025 baada ya swala ya Ijumaa Septemba 12, 2025, miji kadhaa mikubwa ya Sudan ilifanyika visimamo, pamoja na misikiti mikuu ya Sudan yote. Shawak, Singa, Rabak, Madani, Abbasiya, Taqli, Khartoum (Kalakila na Dukhainat), na misikiti miwili mjini Omdurman.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Sudan Wilayah – Mji wa Kosti, Jimbo la White Nile Wakutana na Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party katika Jimbo la White Nile

Mnamo Ijumaa, 12 Septemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilaya ya Sudan ulimtembelea Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party, katika Uwanja wa Azraq Taiba huko Kosti.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan - mbele ya Msikiti Mkuu jijini Port Sudan Wito kwa Watu wa Sudan... Msiiruhusu Amerika Kuichana Nchi Yenu na Kuivua Darfur

Enyi Waislamu: Mataifa katika maisha yao yana masuala nyeti, yaani, masuala ambayo mtu anakuwa na msimamo mmoja: yhai chini yao au kifo kwao. Itikadi ya Uislamu imetubainishia sisi Waislamu masuala yetu nyeti; yaani yale ambayo kipimo chake ni uhai au kifo. Miongoni mwa masuala hayo nyeti ni suala la umoja wa dola na umoja wa Ummah. Tulipoondoa suala hili kwenye kituo chake stahiki hapo awali, Amerika, kwa msaada wa baadhi ya watu wetu, iliweza kuichana nchi yetu na kuitenganisha Sudan Kusini, na sasa inaregea kukamilisha kile ilichoanza mwanzo kuchora, kwa mipaka ya damu, dola mpya katika mabaki ya nchi yetu; kwa kuivua Darfur, ambako matukio yanazidi kupamba moto katika kutumikia njama ya Amerika kwa usaidizi wa zana zake ndani na nje.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail Mjumbe wa Kamati ya Mawasiliano, ulimtembelea Sheikh Onour Muhammad Ahmed, Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan, afisini kwake, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb kutibua njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

Jana, Jumatatu, tarehe 8/9/2025, huko Rabak, mji mkuu wa Jimbo la White Nile, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ulikutana na Sheikh Abdullah Al-Nur Tutu, Imam na Khatib wa Msikiti Mkuu wa Asalaya na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni wa Sudan, Tawi la White Nile, nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo uliongozwa na wafuatao Dkt. Ahmad Mohammad, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Faisal Madani, Abdul Majeed Osman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Ndani ya Muundo wa Kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kuvuruga Mpango wa Kutenganisha Darfur Wanachama wa Hizb ut Tahrir katika Mji wa Al-Obeid Wahutubia Wito Mzito kwa Waislamu katika Msikiti Mkuu wa Al-Obeid na Kubeba Mabango katika Amali Ny

Katika amali mbili tofauti, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumamosi tarehe 06/09/2025, na ndani ya muundo wa kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ya kuvuruga mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Umma ni suala nyeti ambalo kwalo kipimo ni uha na kifo.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nadir Muhammad Hussein, mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, wanachama wa Hizb ut Tahrir, walimtembelea Ustadh Al-Tijani Abdul Wahab, mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan, nyumbani kwake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Ijumaa tarehe 05/09/2025, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Matendo ya Watawala wa Sudan na Misri Kuhusu Bwawa la An-Nahdha Upotevu wa Usalama wa Maji kwa Watu wa Bonde la Nile

Utaratibu wa mashauriano baina ya nchi mbili unaojulikana kama 2+2, unaojumuisha mawaziri wa mambo ya nje na unyunyiziaji maji wa Misri na Sudan, walifanya mkutano katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri mnamo Jumatano, 3/9/2025, kujadili maendeleo katika faili la Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD). Mkutano huo ulisababisha taarifa ya pamoja ambapo pande hizo mbili zilieleza makubaliano yao kamili kuhusu hatari ya hatua za upande mmoja zinazochukuliwa na Ethiopia kuhusu ujazaji na uendeshaji wa bwawa la GERD. Taarifa hiyo iliashiria hatari kadhaa zinazohusishwa na bwawa hilo, ikiwa ni pamoja na dhamana dhaifu ya usalama, mtiririko wa maji usio wa kawaida, na athari zinazoweza kutokea wakati wa ukame.

Soma zaidi...

Maslahi ya Nani Yanatumikiwa kwa Uamuzi wa Serikali wa Kufungua Tena Kivuko cha Mpakani cha Adre huku Watu wa Fashir Wakifa kwa Njaa?!

Serikali ya Sudan ilitangaza mnamo Jumanne kwamba itaongeza muda wa ufunguzi wa kivuko cha mpakani na Chad cha Adre kwa mashirika ya misaada ya kibinadamu hadi mwisho wa mwaka huu. Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa taarifa ikisema kwamba hatua hii inathibitisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kwamba misaada ya kibinadamu inawafikia wale wanaohitaji nchini kote, na kuonyesha nia yake njema katika kuwezesha shughuli za kibinadamu.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Mnaweza Kutibua Mpango wa Kuitenga Darfur, Basi Inukeni Kumtii Mwenyezi Mungu!

Katika hatua inayotarajiwa, kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo, alikula kiapo cha kikatiba kama mkuu wa Baraza la Rais la kile kinachoitwa serikali sambamba huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, mnamo Jumamosi, 30/8/2025. Makamu wa Rais, wajumbe wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu pia walikula kiapo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu