Jumapili, 02 Rajab 1447 | 2025/12/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Mji wa Wad Madani

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ulitembelea Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Jimbo la Al-Jazirah jana, Jumamosi, 13/12/2025. Ujumbe huo uliongozwa na Ustadh Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Abdulaziz Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na mhandisi Walid Kamil.

Soma zaidi...

Je, Vituo vya Mafuta Vina Thamani Zaidi na Hadhi Kubwa Zaidi kuliko Watu?!

Imeripotiwa katika habari kwamba Vikosi vya Ulinzi vya Wananchi wa Sudan Kusini vilianza kupeleka vikosi vyake kulinda Uwanja wa Mafuta wa Heglig kufuatia makubaliano ya pande tatu kati ya Mwenyekiti wa Baraza la Uhuru la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir Mayardit, na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo. Mkuu wa Majeshi ya Wananchi wa Sudan Kusini, Paul Nang, alielezea katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka ndani ya uwanja wa mafuta wa Heglig kwamba makubaliano hayo yalibainisha kuondolewa kwa jeshi na kuondoka kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka kutoka eneo hilo, na alithibitisha kwamba lengo la makubaliano hayo lilikuwa kuhakikisha kwamba hakuna hujuma yoyote inayotokea kwenye vituo vya mafuta!!

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Dkt. Muhammad Al-Umda Hammad

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kwa nyoyo zilizoridhika na amri ya Mwenyezi Mungu, macho yanayobubujika machozi, na huzuni kubwa, inaomboleza mmoja wa mashababu wake aliyebeba ulinganizi wa kuregesha maisha kamili ya Kiislamu; kupitia kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume, Mwenyezi Mungu amsamehe: Dkt. Muhammad Al-Umda Hammad

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Al-Jazirah

Mnamo Jumanne, 2 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Mhandisi Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na akifuatana na Ustadh Omar Ibrahim, pia mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na Mhandisi Walid Kamil, walimtembelea Ustadh Imad Ismail Muhammad Ahmad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Al-Jazirah, afisini kwake Wad Madani.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu

Mnamo Jumatatu, 1 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, walimtembelea Dkt. Imad al-Din Muhammad Hamdallah, mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu, afisini kwake Port Sudan.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Muhadhara wa Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika muhadhara mpya ya Kikao cha Kisiasa, ambao utawasilishwa na Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, wenye kichwa: Mzozo wa Kikoloni barani Afrika - Sudan kama Mfano

Soma zaidi...

Wanamgambo ni Tishio la Usalama kwa Umbo la Serikali, na Uwepo Wao ni Ukiukaji wa Sharia

Mapigano ya silaha yalitokea katika mji wa Dongola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini, jioni ya Ijumaa, 21/11/2025, kati ya vikosi vya jeshi la Sudan na kikundi chenye silaha kinachojulikana kama Awlad Gamri, kaskazini mwa kituo cha usafiri wa miji. Kulingana na kile kilichoripotiwa katika habari, kiongozi wa kikundi hicho, anayeitwa Al-Tom Gamri, alijeruhiwa na kupelekwa hospitalini, na kuna habari za kuuawa kwa mlinzi wake binafsi.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Amerika Inaharakisha Kuvuna Matunda ya Vita vyake nchini Sudan, Kwa hivyo Msiiruhusu Itenganishe Darfur

Wakati wa hotuba yake katika Kikao cha Uwekezaji kati ya Marekani na Saudi Arabia, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Mfalme Mtarajiwa Mohammed bin Salman alikuwa ameomba azimio la mgogoro nchini Sudan, akiongeza kwamba alianza kusoma suala hilo nusu saa tu baada ya maelezo ya Mwanafalme huyo. Trump pia aliandika kwenye tovuti yake ya Kijamii ya Truth kwamba atatumia mamlaka ya urais kusimamisha vita mara moja.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu