Ijumaa, 17 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mtu Anayehusika na Usalama wa Watu Anawezaje Kukimbia Akitafuta Usalama?!

Sudan News ilinukuu Darfur 24 katika ripoti moja yenye kichwa: “Kujiondoa kwa Uratibu au Kuanguka?! Makamanda na Maafisa wa Jeshi na Vikosi vya Pamoja Waondoka Al Fasher Siku Mbili Kabla ya Kuanguka Kwake,” ikisema: “Vyanzo viwili kutoka Darfur Kaskazini viliifichulia Darfur 24 kwamba makamanda wa jeshi, pamoja na wanachama wa vikosi vya pamoja, gavana wa Darfur Kaskazini, Al-Hafiz Bakhit, na wanachama kadhaa wa serikali yake, waliondoka Al Fasher siku mbili kabla ya Vikosi vya Msaada wa Haraka kutangaza udhibiti wao kamili wa makao makuu ya Kikosi cha 6 cha Wanajeshi Wapiganaji.”

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tuna furaha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wale wenye hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao cha kila mwezi cha masuala ya Umma, ambacho mwezi huu kitakuwa kwa kichwa: El Fasher: Kituo Kilicho na Vurugu Zaidi katika Mzozo wa Kimataifa wa Sudan

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamkaribisha Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, chenye kichwa: Msimamo wa Serikali kuhusu Kufutwa kwa Kadhia ya Palestina na Hukmu ya Sharia juu yake.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi 26 Rabi’ al-Akhir 1447 H sawia na 18/10/2025 M Anwani: “Mkanganyiko wa Serikali katika Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu na Athari Zake

Baada ya kujitenga kwa Sudan Kusini mwaka wa 2011, na Sudan kupoteza zaidi ya 75% ya mauzo yake ya nje ya mafuta, dhahabu iliibuka kama njia badali kuu ya kufidia hasara hii na kupata faida kwa fedha za kigeni. Uchimbaji madini ulikuwa umeenea sana nchini Sudan baada ya karibu mwaka wa 2008, na uzalishaji wa dhahabu wa Sudan ukawa mkubwa, na kufikia tani 73.8 mwaka wa 2024, na kushika nafasi ya tano barani Afrika. (AlJazeera.net). Hata hivyo, uzalishaji huu mkubwa haukuinufaisha serikali wala watu; uliporwa na watu binafsi, na makampuni ya kigeni na ya ndani, na hata kile kinachozalishwa kupitia uchimbaji wa jadi hununuliwa na kutolewa kimagendo na baadhi ya makampuni na mashirika. Ili kuthibitisha kile tulichosema kuhusu hili, tunahakiki migodi mikubwa zaidi ya dhahabu nchini Sudan, kwa njia ya mfano na sio kipekee, na jinsi serikali inavyoshughulikia migodi hii!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika ndugu wanahabari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza, wenye kichwa: Mkanganyiko wa Serikali Kuhusu Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu.

Soma zaidi...

Ni lini Tutakomesha Uingiliaji wa Kafiri Magharibi na Mashirika yake ya Kikoloni katika Maisha Yetu, na Kuelekeza Nyuso Zetu Kwa Al-Waahid, Al-Haakim?

Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.

Soma zaidi...

Maradhi ya Mkurupuko Yawaangamiza Watu kwa Kukosekana kwa Dola ya Ustawi

Maradhi matatu ya kimazingira—kipindupindu, homa ya dengue, na malaria—yanawaangamiza watu katika majimbo ya Khartoum, Al-Jazirah, na Darfur, katikati ya uzembe wa kutisha na aibu ya kukosekana kwa serikali inayojiita “Serikali ya Matumaini”! Kuna matumaini aina gani wakati watu wanaishi katika mazingira yasiyostahili hata kwa wanyama—mazingira yanayotawaliwa na waenezaji magonjwa, ikiwemo mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu