Jumatatu, 23 Rajab 1447 | 2026/01/12
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Lazima Tuitupilie Mbali Miungu ya Uongo na Miovu ya Utaifa na Ukabila Kwenye Jaa la Historia!

Kutokana na utaifa, ukabila na kuanzishwa kwa dola za kitaifa na mipaka yake katika ardhi za Waislamu, kitambulisho cha Waislamu kimeharibika na kutengana, ambapo Ummah wa Kiislamu hapo awali uliunganishwa katika udugu mmoja na ndani ya Dola moja ya Kiislamu, badala yake ukagawanyika katika dola za kitaifa zaidi ya 50 na vitambulisho vya kitaifa kufuatia kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342, mikononi mwa Mustafa Kamal, “baba wa udhalifu”.

Soma zaidi...

Dori ya Magharibi Kafiri katika Kuuchana Umma wetu na katika Kuivunja Khilafah yetu, Nembo ya Nguvu Yetu

Tulipokuwa Umma mmoja tofauti na mwingine wowote, dola yetu iliweka Rayah (bendera) yake juu ya maeneo yote; ilikuwa mlinzi, kimbilio, na kizuizi dhidi ya yeyote ambaye angeweza hata kufikiria kumshambulia Muislamu mmoja. Waislamu walikuwa mwili mmoja, wakisaidiana kwa ushindi, msaada, na kuimarishana. Iwapo kiungo kimoja kingelalamika, mwili uliobaki ungejibu kwa kukesha na homa. Kisha maadui walielewa kwamba umoja huu na dola hii ndio sababu ya nguvu ya Umma wa Kiislamu na ngao yake ya kinga. Kwa hivyo walianza kulenga ngao hiyo, wakijaribu kuivua, wakifanya juhudi kubwa kwa miaka mingi mirefu hadi walipofikia lengo lao, kwa masikitiko, na kuivunja Dola ya Khilafah mnamo 1924, wakiuchana Ummah wa Uislamu vipande vipande ili kuizuia kurudi katika hali yake ya zamani.

Soma zaidi...

Rajab na Suala la Umoja wa Waislamu

Kwa Waislamu wengi leo, neno “Khilafah” huhisika kama jambo la mbali. Baadhi hulihusisha na vitabu vya historia, wengine huliona kama jambo la kindoto au lisilo la kawaida. Hili linaeleweka, hasa kwa kizazi ambacho kimewahi kuishi ndani ya mfumo wa kisasa wa dola ya kitaifa. Lakini kila mwaka, mwezi wa Rajab hutukumbusha kimya kimya mabadiliko makubwa katika historia ya Waislamu. Katika Rajab 1924, Khilafah ilifutwa. Huu haukuwa tu mwisho wa serikali, bali kupotea kwa muundo uliopangilia umoja wa Ummah wa Kiislamu kwa zaidi ya karne kumi na tatu.

Soma zaidi...

Kuhutubia Umma katika Mji wa Al-Ubayyid kama Sehemu ya Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Wanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika mji wa Al-Ubayyid walitoa hotuba ya hadhara mnamo siku ya Ijumaa, 13 Rajab 1447 H, sawia na 2 Januari 2026 M, kufuatia swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Soko la Karima Kaskazini. Ustadh Ahmed Wada’a Abdul Karim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza, akielezea kwamba hakuna heshima au usalama isipokuwa chini ya Khilafah. Kisha akahutubia ujumbe kwa wale walio katika nyadhifa za mamlaka na ushawishi, wasomi, wanasiasa, na wanahabari, akiwahimiza kusimama na kufanya kazi ili kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah... Dunia Inajitayarisha Kurudi Kwake

Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Yafanya Mikutano Kadhaa katika Miji mbalimbali nchini Sudan

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, mnamo Rajab 1342 H, na kuukumbusha Ummah kuhusu tukio la kusikitisha lililosababisha Ummah kumpoteza Imam wake, ngao, umoja wake kuvunjika, na kafiri mkoloni kuutawala, kudhibiti maamuzi yake ya kisiasa, kiuchumi, na kijeshi, na kuhamasisha Ummah kufanya kazi ya kuregesha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume

Soma zaidi...

Pindi Uwakilishi Unapokuwa Badali ya Wahyi

Kuapishwa kwa Zohran Mamdani mnamo tarehe 1 Januari 2026, kama wengi kabla yake, kunasherehekewa kama hatua muhimu kwa “uwakilishi wa Waislamu” ndani ya demokrasia ya Magharibi. Hata hivyo, zaidi ya siasa za nembo na utambulisho kuna swali zito zaidi, ambalo linagusa msingi wa itikadi ya kisiasa ya Uislamu: Je, inaruhusiwa kwa Muislamu kushikilia wadhifa wa utunzi wa sheria?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah (Rajab 1342 - Rajab 1447 Hijri)

Sisi katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan tunafuraha ya kuwakaribisha wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Umma cha kila mwezi, ambacho mwezi huu kitakuwa na kichwa: Khilafah Ilivunjwa, na Afya ya Watoto Wetu Ikakiukwa

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu