Jumatano, 07 Muharram 1447 | 2025/07/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya')

Kwa imani kamili juu ya qadhaa ya Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan inaomboleza kwa kuondokewa na mmoja wa wabebaji wake wa Da’wah: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya'), ambaye alifariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu mnamo Alhamisi, tarehe 1 Muharram 1447 H sawia na 26 Juni 2025 M, akiwa na umri wa miaka 89, baada ya kuugua kwa muda mrefu ambapo alikuwa na subira na kwa kutarajia malipo ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Jinsi Dola Kubwa Zinavyozaliwa Utotoni mwao

Ni kweli kwamba dola kubwa hazizaliwi ghafla mara moja, lakini hakuna shaka kwamba zinajengwa juu ya itikadi ambayo kwayo mfumo huchipuka. Wakati wa kuzaliwa kwake, fikra yake ilijumuishwa katika kundi ambalo lilijitolea mhanga mali zake za thamani zaidi na kuiunga mkono kivitendo ndani yake. Hili lilizaa dola yake, ambayo ilijizatiti kujitengenezea njia kuelekea uongozi wa kimataifa kwa msingi wa itikadi yake, kufikia haki na rehema kulingana na viwango vya asili ya kimungu katika miongo michache tu. Ni lazima kwa Ummah ambao kwa hakika unataka kurudisha nafasi yake ya hadhi miongoni mwa mataifa, si tu duniani kote, kuregea kubeba ujumbe wake kwa ulimwengu na kulazimisha uongozi wake wa kifikra na utawala wake juu ya fikra za dhulma, ubabe, na utumwa, na kufikia ukombozi wa kifikra na wa kimada. Umma huu lazima uvuke hisia, mambo ya kijuujuu, na lugha ya maneno hadi vitendo.

Soma zaidi...

Wilayah Tunisia Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ndugu Basheer Qassila

Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia inaomboleza mmoja wa watu wake waliojitolea na wabebaji wa da'wah: mzee na kaka, simba wa da'wah, Basheer Qassila, ambaye alifariki mnamo Jumapili, tarehe 26 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na 22 Juni 2025 M, baada ya kupambana na maradhi yaliyomdhoofisha mwili wake lakini katu hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi pamoja na safu akijitahidi kurudisha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Matembezi yaliyohudhuriwa na umati mkubwa wa watu yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia yalitoka katika mji mkuu wa Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, mnamo tarehe 20 Juni 2025 M kuanzia Msikiti wa Al-Fath chini ya kichwa: “Msafara wa Uthabiti Umesonga, Msafara wa Askari na Uanze!”

Soma zaidi...

Umebarikiwa kwa Nguvu, Umedhoofishwa na Mgawanyiko

"Pentagon yasema Marekani haitaki kuanzisha vita na Iran" - hii, baada ya kudondosha mabomu kumi na nne aina ya bunker-buster kwenye vituo vitatu vya nyuklia ndani ya ardhi ya Iran. Kauli kama hiyo si ya kinafiki tu - ni ya kuchukiza. Inaakisi mawazo ya kiburi, ya kikoloni. Mtu yeyote mwenye akili timamu anawezaje kuamini kwamba vita sio nia pindi taifa linapofanya mashambulizi yaliyoratibiwa kwa taifa jengine?

Soma zaidi...

Vita vya Amerika na umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran: Kimya cha Watawala na Kujisalimisha kwa Murshed

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano kamili kati ya Israel na Iran juu ya usitishaji kamili wa mapigano. Katika jukwaa lake la Kijamii la Truth, Trump alisema: "PONGEZI KWA KILA MTU! Imekubaliwa kikamilifu na kati ya Israel na Iran kwamba kutakuwa na Usitishaji Vita Kamili na Jumla (katika takriban saa 6 kutoka sasa, wakati Israel na Iran zitakapomaliza na kukamilisha misheni zao zinazoendelea, za mwisho!), kwa masaa 12, ambapo Vita vitazingatiwa, VIMEMALIZIKA! Trump alisifu pande zote mbili, akisema: "Misuli, Ujasiri, na Ujasusi kumaliza" mzozo na kusema kwamba ulimwengu na Mashariki ya Kati ndio "WASHINDI halisi".

Soma zaidi...

Erdoğan anapaswa Kuhutubia Umma wenye Ikhlasi na sio Walinzi wa Sykes-Picot kwa Umoja na Udugu wa Kiislamu!

Akihutubia Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu jijini Istanbul, Rais Recep Tayyip Erdoğan ametoa wito wa kuwepo umoja na udugu mkubwa zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu. Erdoğan pia alisema, "Hatutaruhusu kuanzishwa kwa agizo jipya la Sykes-Picot katika eneo letu mipaka kuchorwa kwa damu." Na alisisitiza kwa mara nyengine kwamba suluhisho liko katika "diplomasia na mazungumzo".

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu