Alhamisi, 14 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi Kuhusu Wakristo katika Eneo Hili Mshikamano wa Kudumu kwa Fahamu ya Marekani na Kimagharibi ya “Walio wachache”, iliyo ngeni kwa Watu wa Eneo Hili na Historia Yao!

Katika mahojiano yake na chaneli ya Lebanon Al-Jadeed katika kipindi cha “Huyu ni Mimi” na mwandishi wa habari Samar Abu Khaleel, kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi zinaambatana na ziara ya Papa Leo XIV katika eneo hili, ikiwa ni pamoja na Lebanon, hasa kuhusu suala la kubadilisha utawala wa Syria na kauli yake: “Wakristo wanaondoka Syria leo kwa sababu dola iliyopo ni dola ya Kiislamu! Ingawa haikuwa hivyo wakati wa utawala uliopita...” Na msimamo huu ni uthibitisho wa msimamo uliopita wa Patriarch mwenyewe; ambapo alisema mwaka wa 2011 wakati wa ziara yake nchini Ufaransa chini ya Sarkozy: “Kukiri kwamba makosa na ukiukwaji wa sheria uliotokea nchini Syria hakubatilishi ukweli kwamba Rais Bashar Al-Assad alikuwa ameanza mageuzi, na angepaswa kupewa nafasi”!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Muhadhara wa Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika muhadhara mpya ya Kikao cha Kisiasa, ambao utawasilishwa na Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, wenye kichwa: Mzozo wa Kikoloni barani Afrika - Sudan kama Mfano

Soma zaidi...

Wanamgambo ni Tishio la Usalama kwa Umbo la Serikali, na Uwepo Wao ni Ukiukaji wa Sharia

Mapigano ya silaha yalitokea katika mji wa Dongola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini, jioni ya Ijumaa, 21/11/2025, kati ya vikosi vya jeshi la Sudan na kikundi chenye silaha kinachojulikana kama Awlad Gamri, kaskazini mwa kituo cha usafiri wa miji. Kulingana na kile kilichoripotiwa katika habari, kiongozi wa kikundi hicho, anayeitwa Al-Tom Gamri, alijeruhiwa na kupelekwa hospitalini, na kuna habari za kuuawa kwa mlinzi wake binafsi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Kongamano la Antalya: “Usuli wa Amani na Mustakabali wa Gaza”

Katika kukabiliana na mauaji ya kikatili yanayoendelea (mauaji ya halaiki) yanayofanywa na umbile halifu la Kizayuni dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa, na kutoweka kwa Waislamu zaidi ya 220,000 hadi sasa, Hizb ut-Tahrir / Wilayah Uturuki iliandaa kongamano la pamoja jijini Antalya lenye kichwa: “Usuli wa Amani na Mustakabali wa Gaza.”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Jukwaa la Mazungumzo: “Ni Wakati sasa wa Kituo cha Kisiasa Kujikomboa kutokana na Utegemezi wa Wakoloni wa Magharibi”

Kamati ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia iliandaa jukwaa la mazungumzo lenye kichwa “Ni Wakati sasa wa Kituo cha Kisiasa Kujikomboa kutokana na Utegemezi wa Wakoloni wa Magharibi” siku ya Jumapili, 23 Novemba 2025, katika ukumbi wa mikutano wa hizb katika makutano ya Sukra Ariana katika mji mkuu.

Soma zaidi...

Ni Khilafah Rashida pekee kwa Njia ya Utume ndiyo itakayong'oa Mizizi ya Ukoloni wa Magharibi kutoka Ardhi Zetu

Kwa mwaliko wa Balozi wa Uingereza, Kumar Iyer, pamoja na Ujerumani, Ireland, Uholanzi, na Norway, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilifanya kikao mnamo Ijumaa, 14/11/2025, kuhusu ukiukaji katika mji wa El-Fasher. Baraza hilo lilipitisha kwa kauli moja azimio linaloiamuru Misheni Huru ya Kutafuta Ukweli, ambayo Baraza lilikuwa limeianzisha mnamo 11/10/2023, kuchunguza ukiukaji uliofanywa katika mji huo, ambapo Baraza liliamuru kuwatambua wote waliohusika, ili kusaidia kuwafikisha mbele ya sheria. Na kama mwendelezo wa mbinu yake ya kukataa misheni hii tangu kuanzishwa kwake, Waziri wa Sheria, Abdullah Darf, alitangaza katika mahojiano na tovuti ya habari ya uchunguzi jana, Jumapili 16/11/2025, kwamba “Sudan inakataa kupeleka uchunguzi kuhusu uhalifu wa Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Al-Fashir kwa Kamati ya Kutafuta Ukweli.”

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari yenye kichwa: Makubaliano ya Nchi Nne (Quartet) ya Kusitisha Mapigano na Hatari ya Mazungumzo kwa Msingi wa Hadhara ya Kimagharibi

Tangu Quartet—ambayo inajumuisha sambamba na Amerika, Saudi Arabia na Misri na Imarati, ilipotangaza taarifa yake mnamo 12/9/2025 kuhusu mgogoro wa Sudan, watu wengi nchini Sudan wamegawanywa katika mikondo miwili: mkondo unaounga mkono taarifa ya Quartet inayotaka mazungumzo na suluhisho la kisiasa, kwa kisingizio kwamba inaleta amani, na mkondo mwengine unaosema unakataa kile kilichokuja katika taarifa ya Quartet, na kutaka kuendelea kwa vita. Na ijapokuwa pande zote mbili ni Waislamu, hawakuufanya Uislamu kuwa ndio msingi wa kutoka kwao katika kubainisha misimamo yao, wakati ilitakiwa hapo awali jambo hili litokee

Soma zaidi...

Gaza Inavuna Mavuno Uchungu ya Baraza la Usalama na Uamuzi wa Baraza la Amani

Siku chache baada ya uamuzi wa Baraza la Usalama, watu wa Gaza walianza kuvuna hasara yake; katika muda usiozidi masaa 24, mashahidi 34—wengi wao wakiwa watoto na wanawake—walikuwa wamepanda daraja hiyo hadi kufikia Alhamisi asubuhi, 20/11/2025, pamoja na makumi ya waliojeruhiwa kutokana na uzito wa njaa na kwenye makucha ya baridi kali. Damu hizi safi zilikuwa maana halisi ya uamuzi ulioipa Amerika usimamizi na mamlaka juu ya Ukanda wa Gaza, ikiruhusu kukata vichwa kama ilivyotaka. Ni uamuzi uliopuuza damu, utajiri, na ardhi za watu wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi na kuachilia mkono wa Mayahudi kutumbukia ndani ya damu yetu, ambayo ilienea zaidi ya Gaza hadi Kambi ya Ain al-Hilweh nchini Lebanon.

Soma zaidi...

Abbas, Akizungumza kutoka Pango la Maadui wa Uislamu jijini Paris, Anathibitisha Dori ya Kihalifu ya Mamlaka ya Palestina katika Kutekeleza Sera za Marekani na Mayahudi Zinazolenga Kufuta Kadhia ya Palestina na Kuwakata Watu wa Palestina na Watoto Wa

Katika mkutano kati ya Abbas na Macron jijini Paris mnamo Jumanne, 11 Novemba 2025, ambapo kuundwa kwa kamati ya pamoja ya Ufaransa na Palestina ya kuandika katiba ya dola ya Palestina kulitangazwa (Al Jazeera Mubasher), Abbas anaonekana kupata msukumo kutoka kwa historia ya dola zilizo katika eneo hili zilizopitisha katiba za Magharibi kama msingi wa sheria zao. Wamewachukua Wamagharibi kama mabwana zao, badala ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Abbas hakuweza kufanya chochote ila kugeukia Paris na kuwaomba mabwana zake kuandika katiba ya dola iliyo kwenye karatasi—dola ambayo hawezi kuingia au kutoka bila idhini ya Mayahudi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu