Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 584
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Waislamu ni Ummah mmoja, tofauti na watu wengine; Mola wao Mlezi ni Mmoja, Dini yao ni moja, Mtume wao ni mmoja, Kibla chao ni kimoja, na Kitabu chao ni kimoja.
Hizb ut Tahrir Amerika ilifanikiwa kufanya kongamano lake la kila mwaka kwa mwaka huu 1447 H (2026 M), kama sehemu ya kampeni ya kimataifa iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wao wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).
Hizb ut Tahrir / Amerika ilifanya kwa mafanikio Kongamano lake la kila mwaka la Khilafah kama sehemu ya kampeni ya kimataifa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kufutwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu, kama ulivyoamriwa na Mwenyezi Mungu (swt), kupitia kusimamisha tena Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).
Katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah iliyotokea mnamo Rajab 1342 H / Machi 1924 M, jana, Jumapili, 29 Rajab 1447 H / 18 Januari 2026 m, Hizb ut Tahrir / Tanzania ilifanya semina fupi katika Masjid Taqwa, Ilala Bungoni katika jiji la Dar es Salaam.
Ni sababu gani za udhaifu wa Waislamu leo? Kwa nini heshima yao inavunjwa, ardhi yao inanyakuliwa, na wanamefukarishwa na kutiwa njaa, lakini hawajitetei dhidi ya dhulma, udhalilifu, na kudunishwa? Kwa nini wanatazamana wakifa kwa njaa, mauaji, na mateso mikononi mwa makafiri wahalifu bila kuinua kidole? Kwa nini wanahisi hawana msaada, dhaifu, na watiifu kwa Magharibi mbele ya majanga na vitisho vyote vinavyowapata?
Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon ilifanya kongamano lake la kila mwaka la kisiasa kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”, ambapo wazungumzaji kutoka Lebanon, Syria, Uturuki, na Gaza walishiriki.
Mnamo Jumamosi, tarehe 28 Rajab 1447 H, sambamba na tarehe 17 Januari 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan ilifanya kongamano la kumbukumbu ya miaka 105 tangu kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah. Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mashuhuri, wakiwemo wanasiasa, watu mashuhuri wa vyombo vya habari, wasomi, na viongozi wa jamii. Kwa kuzingatia kwamba kumbukumbu hii chungu inakuja huku sisi nchini Sudan tukiteseka kutokana na vita vilivyowashwa na ubeberu wa Marekani, ikiwatumia vibaraka wake wa ndani kusambaratisha kile kilichobaki cha umoja wa nchi yetu chini ya sera yake inayoitwa “Mipaka ya Damu”. Hivyo, kichwa cha kongamano letu kilikuwa: “Sudan Kati ya Sera za Mipaka ya Damu na Kuunganisha Watu Kuwa Umma Mmoja.”
Kufuatia utekelezaji wa mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan wa visimamo vitatu katika maeneo tofauti tofauti katika jiji la Omdurman, asubuhi ya Jumatano iliyopita, 25 Rajab 1447 H, sambamba na 14/1/2026 M, ndani ya muundo wa kukumbusha tukio la kupita kwa miaka 105 tangu kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mwezi Rajab 1342 H, vyombo vya usalama viliendelea kuwakamata wanachama watano wa Hizb: Al-Radi Muhammad Ibrahim, Fadlallah Ali Suleiman, Omar Al-Bashir, Hassan Fadl, na Mujahid Adam. Kisha waliachiliwa baada ya Magharibi siku ya Jumatano baada ya nambari zao za simu kuchukuliwa na baada ya kunyakua mabango ambayo Mashababu hao wa Hizb ut Tahrir walikuwa wamebeba katika visimamo hivyo vitatu. Kisha waliitwa mnamo alasiri ya Alhamisi, 15/1/2026, na wangali wako kizuizini hadi wakati wa kuandika taarifa hii!!