Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Damu ya Muislamu ni Tukufu Zaidi Kushinda Ka'bah

Khilafah Pekee Ndiyo Itakayolipiza Kisasi cha Damu Hii

(Imetafsiriwa)

Abdullah ibn Umar (ra) amesimulia kwamba alimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akifanya Twawaf katika Ka'bah akisema,

«مَا أَطْيَبَكِ وَأَطْيَبَ رِيحَكِ، مَا أَعْظَمَكِ وَأَعْظَمَ حُرْمَتَكِ، وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَحُرْمَةُ الْمُؤْمِنِ أَعْظَمُ عِنْدَ اللَّهِ حُرْمَةً مِنْكِ؛ مَالِهِ وَدَمِهِ وَأَنْ نَظُنَّ بِهِ إِلَّا خَيْراً»

“Una uzuri ulioje na harufu yako nzuri iliyoje! Una utukufu mkubwa ulioje! Naapa kwa Yule ambaye nafsi ya Muhammad imo mikononi mwake, utukufu wa muumini ni mkubwa Zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wewe (Ka'bah); mali yake na damu yake na tusimdhanie isipokuwa kheri.” (Ibn Majah)

- Serikali ya Hasina daima imekuwa ikikiuka utukufu wa damu ya Waislamu kupitia risasi na mauaji ya kikatili.

- Serikali ya Hasina imewakandamiza watu kupitia chuma na moto kila wanapotaka ima haki yao ya uadilifu au Imani, ikiwemo kupitia mauwaji ya halaiki katika Sapla Chattar, na ukandamizaji wa kinyama wakati wa harakati ya 'Usalama Barabarani'.

- Ukiukaji wa utukufu wa misikiti na utendeaji unyama Waislamu kupitia serikali ya Hasina unaweza tu kulinganishwa na Muuwaji Modi na Umbile nyakuzi la Kiyahudi.

- Khilafah ijayo pekee ndiyo itawaadhibu watawala hawa na kuwalipizia kisasi mashahidi; hivyo, unganeni na harakati ya kusimamisha Khilafah chini ya uongozi wa kweli wa Hizb ut Tahrir.

Enyi Maafisa wenye Ikhlasi wa Jeshi! Kwa vile ambavyo serikali ya Hasina inaendeleza ukandamizaji wa watu kwa chuma na moto, ni jukumu lenu kukomesha udhalimu wake mara moja. Simameni pamoja na watu, na toeni nusrah (usaidizi wa kimada) kwa Hizb ut Tahrir ili kuing'oa serikali hii na kusimamisha Khilafah Rashida

H. 16 Sha'aban 1442
M. : Jumatatu, 29 Machi 2021

Hizb-ut-Tahrir
Wilayah Bangladesh

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.