Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Ripoti ya Habari 18/09/2020

Hizb ut-Tahrir alifanya amali kadhaa katika wiki iliyopita, huku wiki iliyopita ikianza mnamo Septemba 11, 2020 , kwa hotuba kubwa huko Omdurman kaskazini kwa anwani: "Kukubali Usekula kunamaanisha .. kusafisha kile kilichobaki cha hukmu za Uislamu na kuua hisia za Waislamu."

Vile vile, toleo kwa anwani: "Leo Hii Imarati Na Bahrain Zinatia Saini ya Mkataba Pamoja na Dola ya Kiyahudi, Mkataba wa Uhaini Mkuu kwa Palestina Ambayo Ndipo Alipofikia Mtume (saw) Katika Safari Ya Isra Na Miiraj Yake. … Wanafanya Hivyo Hata Bila ya Kumhofu Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na Waumini!," liligawanywa.

Siku ya Jumanne, Septemba 15, 2020 , muhadhara ulifanyika katika eneo la Dukhainat katika Msikiti wa Bilal Bin Rabah kwa anwani: "Sema: Hakika swala zangu, kuchinja kwangu, kuishi kwangu, kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola wa Walimwengu wote."

Vile vile, muhadhara ulifanyika siku ya Alhamisi 17 Septemba 2020 kwa anwani: "Hijra (uhamiaji) ya Mtume ... Mafunzo na Mazingatio" katika Msikiti wa Mapinduzi Moto ya Tisa."

Na mwishoni mwa wiki, siku ya Ijumaa Septemba 18, 2020, hotuba ilifanywa katika eneo la Omdurman kaskazini, na ilikuwa kwa anwani: "Kuanguka kwa pauni na kushindwa kwa serikali ya mpito kuzuia mafuriko ya dolari."

Mwakilishi wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

 katika Wilayah Sudan

Mkusanyiko wa Picha

Imebadilishwa mara ya mwisho mnamoJumamosi, 26 Septemba 2020 14:30

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu